7 Umemufanya kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika. Umemujaza utukufu na heshima.
mutu ni nini, ee Mungu, hata umufikirie? Mwanadamu ni nini hata umujali?
Umemufanya kuwa karibu sawa na Mungu, umemujaza utukufu na heshima.
Lakini kila mutu anayefanya mema atapata utukufu, heshima na amani; kwanza Wayuda, kisha watu wa mataifa mengine vilevile.
Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.
Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.
Lakini mambo tunayoona ndiyo haya: Yesu alifanywa kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika kusudi kwa neema ya Mungu, Yesu akufe kwa ajili ya watu wote. Na sasa kwa njia ya kile kifo kilichomufikia, amepata utukufu na heshima.