Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Ujumbe wa Sheria uliotangazwa na malaika ulitimizwa, na hata kila mutu aliyekosa kuufuata na kuasi aliazibiwa sawa inavyostahili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 2:2
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

mbona unauonea kijicho mulima Mungu aliouchagua akae juu yake? Yawe atakaa huko milele!


Kulikuwa kungali nyama kwa wingi na mbele watu hawajawamaliza kula, Yawe akawakasirikia watu, akawapiga watu kwa pigo kubwa sana.


Hapo Yawe akatuma nyoka wenye sumu kati ya watu, wakawauma hata Waisraeli wengi wakakufa.


Waliokufa kutokana na ugonjwa ule mukali walikuwa watu elfu makumi mbili na ine.


Mungu aliwatolea ninyi Sheria yake kwa njia ya wamalaika, lakini hamukuitii.”


Basi Sheria iko na kazi gani? Ilisimamishwa nyuma kwa ajili ya kutambulisha makosa. Nayo ilipaswa kuendelea mpaka atakapokuja yule muzao wa Abrahamu ambaye Mungu alikuwa ameahidi. Sheria hii ilitangazwa na malaika kwa njia ya mupatanishi.


Naye mutu atakayetenda kwa kiburi bila kutii kuhani aliyewekwa hapo kwa kumutumikia Yawe, Mungu wenu, au mwamuzi, mutu huyo atauawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.


“Kama mukisikia katika mumoja wa miji yenu kuna mwanaume au mwanamuke anayetenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wenu, na kuvunja agano lake


basi, mumupeleke mutu huyo inje ya miji na kumupiga mawe mpaka akufe.


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote asiyekubali maneno haya ya sheria na kuyatii’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Mafundisho yangu yatone kama mvua, maneno yangu yadondoke kama umande, kama manyunyu kwenye mimea michanga, kama mvua nyepesi katika majani mabichi.


Zamani Mungu alisema na babu zetu kwa njia ya manabii, mara nyingi na kwa namna nyingi.


Mutu yeyote aliyevunja Sheria ya Musa, aliuawa bila huruma kisha ushuhuda wa watu wawili au watatu.


Basi musikate tumaini, kwa maana litawaletea zawadi kubwa.


Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake.


Basi pasipo imani, hakuna mutu anayeweza kumupendeza Mungu. Kwa maana mutu anayetaka kumwendea Mungu sherti aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba anawapa zawadi wale wanaomutafuta.


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.


Ijapokuwa mumekwisha kujua kabisa mambo haya yote, ninataka kuwakumbusha namna Bwana alivyowaokoa Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri, lakini kisha, akawaangamiza wale waliokataa kuamini.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ