Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 2:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 2:17
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, wale makuhani wakawachinja, na kunyunyiza damu yao juu ya mazabahu kusudi ikuwe sadaka ya upatanisho kwa Waisraeli wote, kwa maana mufalme Hezekia alikuwa ameagiza sadaka ya kuteketeza kwa moto na sadaka ya maondoleo itolewe kwa ajili ya Waisraeli wote.


Haki itakuwa kama mukaba wa kujifunga, uaminifu utakuwa kama mukaba kwenye kiuno chake.


Watatoa kondoo mumoja kwa kila kundi la kondoo mia mbili katika jamaa za Waisraeli. Wataleta sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani, kusudi wapate kufanyiwa upatanisho. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Itakuwa ni mapaswa ya mufalme kuhakikisha kuwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za vyakula na sadaka za kinywaji zinazotolewa wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi, Sabato, na sikukuu zozote zilizowekwa kwa Waisraeli, zinapatikana. Mufalme yeye mwenyewe atatayarisha sadaka za kusamehewa zambi, sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani kwa kuwafanyia watu wote wa Israeli upatanisho.


Atafanya vile vile siku ya saba ya mwezi huo, kwa ajili ya kila mutu aliyetenda zambi bila kukusudia au kwa kutokujua. Kwa njia hiyo mutaitakasa nyumba ya Yawe.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Yale mafuta yaliyobaki atayapakaa yule mutu kwenye kichwa. Hivyo kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe.


Hivyo atafanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya Pahali Patakatifu kwa sababu ya uchafu, makosa na zambi zote za Waisraeli. Ndivyo atakavyofanya vilevile kwa ajili ya hema la mukutano linalokuwa kati ya watu hao wanaokuwa wachafu.


Musa akamuchinja huyo ngombe, akatwaa damu akapakaa pembe za mazabahu pande zote kwa kidole chake kwa kuitakasa. Kisha akatwaa damu iliyobaki akaimwanga chini kwenye tako la mazabahu ambayo alitakasa kwa kuifanyia ibada ya upatanisho.


Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya Waisraeli wote pamoja, nao watasamehewa kwa sababu si kosa lililokusudiwa, na wameleta sadaka yao, sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe kama sadaka ya zambi kwa ajili ya kosa lao.


Basi katika kuungana kwangu na Kristo, ninaweza kujisifu kwa ajili ya kazi hii ninayomutumikia Mungu.


Basi ikiwa kama tulipokuwa waadui za Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kufa kwa Mwana wake, inaonyesha zaidi sana kwamba tukiwa tumepatanishwa naye, tutaokolewa kwa njia ya uzima wa Kristo.


Kristo alivunja uadui kwa njia ya kufa kwake juu ya musalaba, akaunganisha watu wa makabila haya mawili kuwa moja na kuwapatanisha na Mungu.


Na ninyi zamani mulikuwa mbali na Mungu, mulikuwa waadui zake kwa sababu ya mafikiri na matendo yenu mabaya.


Sisi tuko na Kuhani Mukubwa anayesimamia nyumba yote ya Mungu.


Yeye anawatakasa watu toka katika zambi, na wale wanaotakaswa naye, wote ni watoto wa Baba mumoja. Ni kwa sababu hiyo Yesu hasikii haya ya kuwaita wandugu zake.


Basi kwa kuwa hao watoto ni wanadamu, wenye mwili na damu, Yesu vilevile alitwaa ile hali ya mwanadamu. Alifanya hivi kusudi kwa njia ya kufa kwake amwangamize Shetani aliyekuwa na uwezo wa kuleta lufu.


Kwa maana hakika hakukuja kuwasaidia wamalaika, lakini alikuja kuwasaidia wazao wa Abrahamu.


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


Yeye alikuwa mwaminifu mbele ya Mungu aliyemusimika kwa kazi ile, sawa vile Musa alivyokuwa mutumishi mwaminifu katika kazi ya nyumba yote ya Mungu.


Musa alikuwa mutumishi mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, kusudi ashuhudie maneno ambayo Mungu angesema nyuma.


Basi, kwa kuwa tuko na Kuhani Mukubwa zaidi aliyeingia mbinguni, ndiye Yesu Mwana wa Mungu, tushikamane sana na imani tunayotangaza.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Kila Kuhani Mukubwa aliyechaguliwa kati ya watu amesimikwa kwa kumutumikia Mungu kwa ajili ya watu kusudi atolee matoleo na sadaka kwa ajili ya zambi.


Basi, Mungu alitangaza kwamba yeye ni Kuhani Mukubwa kwa mufano wa Melkisedeki.


Kwa kuwa yeye mwenyewe ni muzaifu, anaweza kuwavumilia wale waliopotoka bila kujua.


Hivi vilevile, Kristo hakujipatia yeye mwenyewe utukufu wa kuwa Kuhani Mukubwa, lakini ni Mungu ndiye aliyemwambia: “Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.”


Yesu alitangulia kuingia pahali pale kwa ajili yetu. Amekuwa Kuhani Mukubwa hata milele, kwa mufano wa Melkisedeki.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Sheria ya Musa inawaweka watu wenye uzaifu kuwa Makuhani Wakubwa, lakini kufuatana na kiapo kilichokuja nyuma ya Sheria ile, Mwana anayekuwa mukamilifu kwa milele aliwekwa kuwa Kuhani Mukubwa.


Jambo la lazima sana katika maneno tunayosema sasa ni hili. Tuko na Mukubwa wa namna ile, anayeikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mwenyezi Mungu.


Kila Kuhani Mukubwa anawekwa kusudi afanye kazi ya kutoa sadaka na matoleo. Kufuatana na hiyo, ilimupasa Kuhani wetu Mukubwa Kristo akuwe na kitu cha kutoa vilevile.


Lakini Kristo alikuja kuwa Kuhani Mukubwa anayeshugulika na mambo mema ambayo sasa yamekwisha kutokea. Yeye alipita katika hema inayokuwa bora zaidi na kamilifu. Hema hii haikutengenezwa na watu, maana yake si ya dunia hii.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ