Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Yeye anawatakasa watu toka katika zambi, na wale wanaotakaswa naye, wote ni watoto wa Baba mumoja. Ni kwa sababu hiyo Yesu hasikii haya ya kuwaita wandugu zake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 2:11
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Kisha Yesu akawaambia: “Musiogope, muende kuwaambia wandugu zangu waende Galilaya, na kule wataniona.”


Kisha akawaangalia watu waliomuzunguka, na kusema: “Mama yangu na wandugu zangu, ni hawa wanaoikaa hapa.


Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu kati ya watu wa kizazi hiki kisichokuwa na uaminifu mbele ya Mungu na chenye zambi, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile, atakapokuja pamoja na wamalaika watakatifu, akitukuzwa na Baba yake.”


Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile atakapokuja katika utukufu wake, akitukuzwa na Baba yake pamoja na wamalaika wake watakatifu.


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.


Yesu akamwambia: “Usinishike, kwa sababu sijapanda bado kwa Baba. Lakini kwenda kwa wandugu zangu na kuwaambia kwamba ninapanda kwa Baba yangu anayekuwa Baba yenu vilevile, anayekuwa Mungu wangu na Mungu wenu vilevile.”


Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.


maana ‘kwa uwezo wake tunaishi, tunatenda na kuendelea kuwa.’ Ni sawa na maneno ya watunga mashairi wamoja wa kwenu waliosema: ‘Sisi vilevile tuko watoto wake.’


Kwa maana wale Mungu aliowachagua tangu zamani, ndio aliofanya mupango juu yao tangu zamani, apate kuwafananisha na Mwana wake, kusudi Mwana wake akuwe muzaliwa wa kwanza wa wandugu wengi.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Na kwa sababu Yesu Kristo alifanya mapenzi ya Mungu, sisi tumetakaswa zambi kwa njia ya mwili wake alioutoa sadaka kwa mara moja tu.


Kwa maana kwa njia ya sadaka moja aliyotoa, amewafanya wale aliowatakasa kuwa wakamilifu hata milele.


Lakini kwa hakika walitamani sana inchi inayokuwa bora zaidi, ndiyo inchi ya mbinguni. Kwa sababu hii Mungu hasikii haya kuitwa Mungu wao, maana amewatayarishia muji.


Kwa sababu hii Yesu vilevile aliuawa mbali na muji kusudi awatakase watu wake kwa njia ya damu yake mwenyewe.


Basi kwa kuwa hao watoto ni wanadamu, wenye mwili na damu, Yesu vilevile alitwaa ile hali ya mwanadamu. Alifanya hivi kusudi kwa njia ya kufa kwake amwangamize Shetani aliyekuwa na uwezo wa kuleta lufu.


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ