Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 13:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Muwasalimie waongozi wenu wote na watu wote wa Mungu. Wandugu wa Italia wanawasalimia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 13:24
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kule akakutana na Muyuda aliyeitwa Akila, muzaliwa wa jimbo la Ponto, na jina la muke wake lilikuwa Prisila. Katika siku zile walikuwa wangali wakitoka katika inchi ya Italia, kwa sababu mutawala Klaudio alikuwa ameamuru kwamba Wayuda wote watoke Roma. Paulo akaenda kuwatembelea kwao.


Walipokwisha kukamata mupango wa kutusafirisha kwa njia ya chombo mpaka Italia, wakamuweka Paulo na wafungwa wengine chini ya uangalizi wa mukubwa mumoja wa waaskari aliyeitwa Yulio. Yeye alikuwa wa kundi la waaskari lililoitwa “Kundi la waaskari wa mufalme.”


Anania akajibu: “Bwana, nimekwisha kusikia watu wengi wakisema habari za mutu huyo, wakieleza mabaya aliyowatendea watu wako watakatifu wanaokuwa Yerusalema.


mukubali kuongozwa na watu kama hawa na wale wote wanaotumika na bidii pamoja nao.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo. Mimi ambaye kwa mapenzi ya Mungu, niliitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu. Tunawaandikia kanisa la Mungu linalokuwa Korinto na watu wake wote wanaokuwa katika jimbo lote la Akaya.


Tunawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana Yesu Kristo, na upendo wa Mungu na ushirika wa Roho Mutakatifu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.


Watu wote wa Mungu, na hasa zaidi wale wanaokuwa katika nyumba ya Mufalme, wanawasalimia vilevile.


Tunawaandikia ninyi watu wa Mungu munaokaa katika muji Kolosayi, ninyi wandugu munaoungana na Kristo kwa uaminifu. Tunawatakia neema na amani toka kwa Mungu Baba yetu.


Kwa maana ninasikia namna unavyomwamini Bwana Yesu na namna unavyowapenda watu wote wa Mungu.


Mutii waongozi wenu na kushika maagizo yao. Kwa maana wao wanashugulika kila mara kwa ajili ya roho zenu, na wao wanapaswa kutoa habari ya kazi yao mbele ya Mungu. Kwa kufanya vile mutawaruhusu kufanya kazi yao kwa furaha wala si kwa huzuni, kwa maana haitawafalia kitu kama wakitumika katika huzuni.


Muwakumbuke waongozi wenu waliowatangazia neno la Mungu. Muangalie vizuri namna walivyoishi na kufa. Mufuate imani yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ