Paulo akawakazia macho wale washauri wa Baraza Kubwa na kusema: “Wandugu zangu, mpaka leo zamiri yangu hainihukumu juu ya kitu chochote kinachoelekea mwenendo wangu mbele ya Mungu.”
Wandugu zangu, ninawasihi kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo na kwa ajili ya upendo unaoletwa na Roho wa Mungu, muungane nami kwa kuniombea kwa Mungu.
Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.
Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.
Mutuombee sisi vilevile kusudi Mungu atufungulie njia ya kuhubiri neno lake tupate kutangaza ujumbe wa siri juu ya Kristo. Ni kwa ajili ya ujumbe ule mimi niko sasa katika kifungo.
Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.
Maji haya ni mufano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo ule si kwa ajili ya kusafisha uchafu wa mwili lakini ni njia ya kufanya mapatano na Mungu katika zamiri safi. Nao unawaokoa ninyi kwa njia ya ufufuko wa Yesu Kristo,