Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 13:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Basi kwa njia ya Yesu, tumutolee Mungu sadaka za kumusifu siku zote, maana yake kutangaza kwamba tunaaminia jina lake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 13:15
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Hezekia akawaambia watu: “Sasa mumekwisha kujitakasa, mukaribie, mulete sadaka na matoleo ya shukrani katika nyumba ya Yawe.” Basi, watu wakaleta sadaka zao na matoleo yao ya shukrani, na za kuteketeza.


Akarudisha mazabahu ya kumwabudia Yawe, na juu yake akatoa sadaka za amani na za shukrani, akawaamuru watu wa inchi ya Yuda wamwabudu Yawe, Mungu wa Israeli.


Makuhani walikuwa wakisimama kwenye nafasi za kazi zao, nao Walawi, walisimama wakiwa na vyombo vya Yawe vya muziki mufalme Daudi alivyotengeneza kwa ajili ya kutoa shukrani kwa Yawe. Waliimba: “Wema wake unadumu milele.” Wakati Daudi alipotoa shukrani, walimusaidia; makuhani walipiga baragumu nao Waisraeli wote wakasimama.


Wakaimba kwa kupokezana, wakimusifu na kumutukuza Yawe: “Yeye ni muzuri, wema wake kwa Waisraeli unadumu milele.” Watu wote walipaza sauti kwa nguvu zao zote, wakamusifu Yawe kwa sababu ya kuanza kujenga musingi wa nyumba ya Yawe.


Hivyo, makundi yote mawili yaliyokuwa yanaimba nyimbo za shukrani yakasimama katika nyumba ya Mungu, pamoja nami na nusu ya viongozi;


Siku hiyo, watu wakatoa sadaka nyingi na kufurahi maana Mungu aliwafanya kuwa na furaha kubwa. Vilevile wanawake na watoto, wote wakafurahi. Vigelegele vya furaha toka katika Yerusalema vikasikilika mbali.


Munifungulie milango ya watu wa haki, niingie na kumushukuru Yawe!


Ee Yawe, upokee maombi yangu ya shukrani, na kunielezea maamuzi yako.


Ameniokoa kutoka waadui zangu, Ee Yawe, ulinitukuza juu ya wapinzani wangu na kuniponyesha kutoka watesaji wakali.


Shukrani ikuwe ndiyo sadaka yako kwa Mungu. Umutimizie Mungu Mukubwa ahadi zako.


Anayenitolea shukrani kama sadaka yake, huyo ndiye anayenitukuza; yeyote anayedumu katika njia yangu, huyo ndiye nitakayemwokoa.”


Mimi nitawapa amani, amani kwa wanaokuwa mbali na wanaokuwa karibu! –Ni Yawe anayesema hivyo.– Mimi nitawaponyesha.


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Vilevile nao makuhani wa ukoo wa Lawi watakuwa pale siku zote kwa kunitumikia wakinitolea sadaka za kuteketezwa na sadaka za unga na kunitolea sadaka milele.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Ikiwa mutu anatoa sadaka hiyo kwa kumushukuru Mungu, basi, ataitoa pamoja na maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopakwa mafuta, mikate myembamba iliyopakwa mafuta na maandazi ya unga laini uliochanganywa na mafuta.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Saa ile ile, Yesu akajazwa na furaha kwa uwezo wa Roho Mutakatifu, naye akasema: “Ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo. Ndiyo Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.


Mimi ni mulango. Mutu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata chakula.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Basi wandugu zangu, kufuatana na vile Mungu alivyoonyesha huruma yake kwetu, ninawasihi mujitoe wenyewe kwake kuwa sadaka yenye uzima, takatifu na yenye kumupendeza. Hii ndiyo njia ya kweli ya kumwabudu.


(Ninatumia luga ya kawaida ya wanadamu kwa sababu ya uzaifu wenu wa kimutu). Zamani mulijitoa kabisa kuwa watumwa wa kufanya mambo machafu na maovu kwa kuishi katika machafuko. Hivi vilevile mujitoe kabisa kuwa watumwa wa kufanya haki kusudi muweze kuishi katika utakatifu.


Kwa maana, kwa njia ya Kristo sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, tumefunguliwa njia ya kufika mbele ya Baba katika Roho mumoja.


mumushukuru Mungu Baba aliyewawezesha ninyi kuwa wenye kustahili kupokea sehemu yenu ya urizi aliowawekea watu wake katika ufalme wa mwangaza.


Basi kwa kuwa tunakubaliwa kuwa washiriki wa ufalme usioweza kutikiswa, tukuwe watu wenye shukrani. Tuonyeshe shukrani ile kwa kumwabudu Mungu kwa njia inayomupendeza kwa heshima na woga,


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


Yule anayehubiri, anapaswa kutoa ujumbe wa Mungu. Na yule anayetumika, atumike kwa kadiri ya nguvu alizopewa na Mungu, kusudi Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo anayekuwa mwenye utukufu na uwezo kwa milele na milele. Amina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ