Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 13:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kwa maana hapa katika dunia hatuna muji unaodumu, lakini tunatazamia muji ule unaokuja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 13:14
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Musimame! Muende! Hapa hakuna tena pahali pa kupumzika! Kwa ajili ya ukosefu wenu wa uaminifu, maangamizi makubwa yanawangojea!


Wandugu zangu, mimi ninataka kusema hivi: wakati uliopangwa unabaki mufupi. Tangu sasa wale waliooa waishi kama vile wasiooa.


Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.


Basi sasa, ninyi watu wa mataifa mengine si wageni tena wala wapangaji. Lakini sasa mumekuwa wanainchi pamoja na watu wa Mungu na tena mumekuwa watu wa jamaa la Mungu.


Lakini sisi ni wenyeji wa mbingu, tunamungojea Mwokozi wetu Bwana Yesu Kristo, afike kutoka kule.


Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.


Neno hili “mara moja tena” linaonyesha kwamba vitu vilivyoumbwa vitatikiswa na kutoweka, kusudi vile visivyoweza kutikiswa vipate kudumu.


Mungu hakuwapa wamalaika uwezo wa kutawala ulimwengu unaokuja, ndio ule tunaosema juu yake.


Kwa hiyo kungali mapumziko ambayo Mungu anawatayarishia watu wake.


Lakini Kristo alikuja kuwa Kuhani Mukubwa anayeshugulika na mambo mema ambayo sasa yamekwisha kutokea. Yeye alipita katika hema inayokuwa bora zaidi na kamilifu. Hema hii haikutengenezwa na watu, maana yake si ya dunia hii.


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Yule atakayeshinda nitamufanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, naye hatatoka tena mule. Na zaidi ya ile nitaandika juu yake jina la Mungu wangu na jina la muji wa Mungu wangu, ndio Yerusalema mupya, utakaoshuka toka mbinguni kwa Mungu wangu. Nitaandika vilevile juu yake jina langu jipya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ