Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 12:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Mumefikia karibu na Yesu anayekuwa mupatanishi wa agano jipya, na kwenye damu yake iliyomwangwa inayosema nasi maneno mema zaidi kuliko damu ya Abeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 12:24
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akasema: “Umefanya nini? Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo.


Musa akatwaa ile damu na kuwanyunyizia watu, akisema: Hii ndiyo damu ya agano ambalo Yawe amefanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Kisha, atamuchinja huyo ngombe mbele ya Yawe. Nao makuhani wazao wa Haruni wataichukua damu na kuinyunyizia mazabahu inayokuwa kwenye mulango wa hema la mukutano, pande zake zote.


Na hivi mutabeba lazima ya damu iliyomwangwa katika dunia pasipo kosa, tangia kuuawa kwa Abeli aliyekuwa mukamilifu mpaka kuuawa kwa Zakaria, mwana wa Barakia, muliyemwuia kwenye hekalu katikati ya Pahali Patakatifu na mazabahu.


kwa maana hii ni damu yangu inayomwangika kwa ajili ya wengi kusudi wasamehewe zambi. Nayo damu hii inahakikisha agano la Mungu.


Na Yesu akawaambia: “Hii ni damu yangu; damu inayomwangika kwa ajili ya watu wengi kwa kuhakikisha agano la Mungu.


tangia kuuawa kwa Abeli mpaka kuuawa kwa Zakaria kwenye hekalu katikati ya mazabahu na Pahali Patakatifu. Kweli ninawaambia: watu wa kizazi hiki watabeba lazima ya mambo hayo yote.


Vilevile kisha kula akatwaa kikombe na kuwapa akisema: “Kikombe hiki ni agano jipya la Mungu, linalohakikishwa kwa njia ya damu yangu.]


Lakini ikiwa jambo linaelekea mutu mumoja tu, si lazima kuwa na mupatanishi; na Mungu ni mumoja tu.


Kwa maana kuna Mungu mumoja tu, na kuna mupatanishi mumoja tu kati ya Mungu na watu, ni yule mutu, Kristo Yesu,


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Kwa njia ya imani, alianzisha sikukuu ya Pasaka, na kuamuru damu inyunyizwe, kusudi malaika mwangamizaji asiwaue wazaliwa wa kwanza wanaume wa Waisraeli.


Kwa njia ya imani, Abeli alimutolea Mungu sadaka nzuri zaidi kuliko ile ya Kaina. Kwa ajili ya imani yake alihesabiwa na Mungu kuwa mwenye haki, kwa maana Mungu mwenyewe alikubali sadaka zake. Na kwa imani ile, ingawa Abeli amekwisha kufa, angali anasema.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Kwa sababu ya kiapo hiki, Yesu amekuwa kihakikisho kwetu cha agano linalokuwa zuri zaidi.


Mungu alipotangaza hilo agano kuwa “jipya”, jambo hilo lilisababisha lile la kwanza kuwa la zamani na lenye kuchakaa. Na kitu chochote kikiwa cha zamani na chenye kuchakaa kinafikia wakati wa kutoweka.


Lakini sasa Yesu amepewa kazi inayokuwa bora zaidi kuliko kazi ya wale makuhani, kwa maana yeye ni mupatanishi wa agano linalokuwa zuri zaidi. Sherti za agano lile zinasimamia juu ya ahadi ya Mungu inayokuwa bora zaidi.


Lakini Mungu aliwaonya watu wake, akisema: “Katika siku zinazokuja, nitafanya agano jipya na watu wa ufalme wa Israeli na wa Yuda. Ni Bwana anayesema hivyo.


Kwa sababu hii, Kristo ni mupatanishi wa agano jipya. Kwa njia ya kufa kwake aliwakomboa watu toka katika makosa waliyofanya chini ya uongozi wa agano la kwanza, kusudi wale walioalikwa na Mungu wapate kupokea urizi wa milele aliowaahidia.


Kwa maana, kwanza Musa aliwatangazia watu wote amri zote za Sheria. Kisha akatwaa damu ya ngombe pamoja na maji, naye akavinyunyiza juu ya kitabu cha Sheria na juu ya watu wote akitumia manyoya mekundu na vitawi vya muti wa hisopo.


Musa akanyunyiza vilevile damu juu ya Hema na juu ya vyombo vyote vya ibada.


Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ