Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 12:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Lakini ninyi mumefikia kwenye mukutano wa furaha wa wazaliwa wa kwanza wa Mungu walioandikwa majina zao katika mbingu. Mumefikia vilevile karibu na Mungu, anayekuwa mwamuzi wa watu wote na kwenye nafsi kunapokuwa roho za watu wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 12:23
45 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”


Haleluia! Nitamushukuru Yawe kwa moyo wangu wote, katika mukutano wa watu wa usawa.


Uwaazibu kwa kila uovu wao; ukatae kabisa kuwasamehe.


Yeye atasema, ‘Wewe ni baba yangu, Mungu wangu, mulima wa wokovu wangu.’


Nani katika mbingu anayeweza kulinganishwa nawe, ee Yawe? Nani anayekuwa sawa nawe kati ya miungu?


Usimame, ee mwamuzi wa watu wote; uwaazibu wenye kiburi inavyowastahili!


mbele ya Yawe kwa sababu anakuja. Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki, na mataifa kwa uaminifu wake.


Mushangilie mbele ya Yawe, maana anakuja kutawala dunia. Atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kama vile inavyofaa.


“Unitakasie wazaliwa wote wa kwanza, maana wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli ni wangu, ikuwe wanaume au wanyama.”


Lakini sasa, ninakuomba uwasamehe zambi yao. Ikiwa hautawasamehe, ninakusihi unifute mimi katika kitabu chako ambamo uliwaandika watu wako.


Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.


mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.


Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.


Hata hivi musifurahi kwa sababu pepo wanawatii, lakini mufurahi kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”


Vilevile amemupa Mwana mamlaka ya kuhukumu, kwa sababu yeye ni Mwana wa Mutu.


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi.


Na kama vile tulivyofanana na yule mutu aliyeumbwa kwa udongo, vilevile tutafanana na yule aliyetoka mbinguni.


Na wakati mwili huu wa kuharibika utakapovaa ule wa kutoharibika, nao mwili wa kufa utakapovaa ule wa kutokufa, halafu Maandiko Matakatifu haya yatatimia: “Kifo kimekomeshwa; kimeshindwa kabisa.”


Sisi tuna uhodari na tungependa zaidi kutoka katika mwili huu na kwenda kuishi pamoja na Bwana.


Mungu amemupatia Kristo mamlaka juu ya vitu vyote na kumuweka kuwa kichwa cha kanisa.


Anapaswa kukubali yule muzaliwa wa kwanza, mutoto wa yule mwanamuke asiyependwa, na kumupa haki yake: sehemu ya mali zake mara mbili.


Na wewe vilevile mutumishi mwenzangu mwaminifu, ninakuomba uwasaidie wanawake hao, kwa maana walisumbuka sana pamoja nami katika kazi ya kutangaza Habari Njema. Kuko vilevile Klementi na wenzangu wengine wa kazi. Hao wote majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.


mumushukuru Mungu Baba aliyewawezesha ninyi kuwa wenye kustahili kupokea sehemu yenu ya urizi aliowawekea watu wake katika ufalme wa mwangaza.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Kwa maana mutu anayeshindwa na kuongoza jamaa yake mwenyewe, namna gani ataweza kuchunga kanisa la Mungu?


Kwa njia ya imani, Abeli alimutolea Mungu sadaka nzuri zaidi kuliko ile ya Kaina. Kwa ajili ya imani yake alihesabiwa na Mungu kuwa mwenye haki, kwa maana Mungu mwenyewe alikubali sadaka zake. Na kwa imani ile, ingawa Abeli amekwisha kufa, angali anasema.


kwa maana Mungu alikuwa ametayarisha mambo mazuri zaidi kwa ajili yetu kusudi wao wenyewe wasipate kukamilishwa bila sisi vilevile.


Kwa maana anasema: “Ee Mungu, nitatangaza jina lako kwa wandugu zangu, nitakusifu katikati ya mukutano.”


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Kwa mapenzi yake mwenyewe alitupatia sisi uzima kwa njia ya ujumbe wa kweli, kusudi tupate kuwa kama mavuno ya kwanza katikati ya viumbe vyake.


Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


Wakaaji wote wa dunia watamwabudu, ndio wale wote ambao tangia kuumbwa kwa dunia, majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.


Watu wale ndio waliojilinda katika usafi bila kujichafua kwa kulala na wanawake, nao wanamufuata Mwana-Kondoo kila fasi anapokwenda. Wamekombolewa kati ya watu wengine kusudi wakuwe wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo kama vile sadaka ya mavuno ya kwanza.


Na mutu yeyote ambaye jina lake lililokosa kuandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto.


Kila mumoja wao akapewa kanzu nyeupe, wakaambiwa wapumzike kwa muda kidogo mpaka wakati hesabu ya watumishi wenzao na wandugu watakaouawa vilevile kama wao itakapotimia.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tano, nikaona chini ya mazabahu, roho za watu waliouawa kwa sababu ya kutangaza Neno la Mungu na kwa sababu ya ushuhuda wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ