Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 12:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 12:14
48 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yakobo akamwambia: “Tafazali, ninakuomba uniambie jina lako.” Lakini yeye akamwambia: “Kwa nini kuniuliza jina langu?” Kisha akamubariki Yakobo.


Na nyuma ngozi yangu kuharibika hivyo, nitamwona Mungu nikiwa na mwili huu.


Kisha atamwomba Mungu na kukubaliwa, atakuja mbele yake kwa furaha, na Mungu atamurudishia utukufu wake.


Nimeishi muda murefu sana kati ya watu wanaochukia amani!


Wimbo wa safari za kidini: wa Daudi. Ni jambo zuri na la kupendeza sana kwa ndugu kuishi pamoja kwa umoja.


Basi, uache kusema mabaya, na kuepuka kusema uongo.


Waadui zangu ni wazima, wana nguvu, ni wengi sana hao wanaonichukia bure.


Maana hukumu zitatolewa kwa haki tena, na wote wenye moyo wa usawa watazifuata.


Kujibu kwa upole kunatuliza hasira, lakini neno kali linachochea hasira.


Yawe akipendezwa na mwenendo wa mutu, anawageuza hata waadui zake kuwa warafiki.


Kuanzisha ugomvi ni kama kufungua maji ya kisima; achana na ugomvi mbele haujafurika.


Yawe anasema hivi: Munisikilize enyi munaotaka kukombolewa, ninyi munaonitafuta mimi Yawe. Muangalie jiwe mulilochongwa toka ndani yake, mulima mulimochimbuliwa.


“Chumvi ni kitu kizuri. Lakini chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini kusudi ipate tena kukolea? “Muwe na chumvi ndani yenu na muishi pamoja kwa amani.”


katika hali ya utakatifu na haki mbele yake siku zote za maisha yetu.


Kama ikiwezekana, kwa upande wenu, muishi katika amani na watu wote.


Basi kwa hiyo tujikaze sana kufanya mambo yale yanayoleta amani na yanayotusaidia kujengana katika imani.


Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.


Wandugu zangu, ninawasihi ninyi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mukuwe na masikilizano kusudi matengano yasikuwe katikati yenu. Muishi katika umoja kabisa mukiwa na nia moja na wazo moja.


Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi.


Kwa sababu hiyo Bwana anasema: “Mutoke kati yao, mujitenge nao. Musiguse kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, nami nitawapokea.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Basi, ni kusema kwamba Sheria haipatani na ahadi za Mungu? Hapana, hata kidogo! Kama kungetolewa Sheria yenye uwezo wa kuleta uzima kwa watu, basi mutu angehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria.


Mujue waziwazi kwamba mwasherati yeyote na muchafu na mwenye tamaa ya mali (mwenye tamaa ni kama mwenye kuabudu sanamu), hao wote hawatapewa sehemu ya urizi katika Ufalme wa Kristo na Mungu.


Sitaki kusema kwamba nimekwisha kufikia mwisho au kwamba nimekwisha kuwa mukamilifu. Lakini ninakaza mwendo kusudi nipate kushinda na kupokea zawadi, kwa maana Yesu Kristo amekwisha kunipokea nikuwe wake.


Vilevile aitie mioyo yenu nguvu nanyi mutapata kuwa watakatifu na bila kosa mbele ya Mungu Baba yetu siku Bwana wetu Yesu atakaporudia pamoja na watakatifu wake wote.


Kwa maana Mungu hakutuita kusudi tuishi katika uchafu, lakini katika utakatifu.


Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.


Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.


Wababa zetu wa kimwili walituadibisha kwa siku chache kufuatana na vile walivyoona kuwa vema. Lakini Mungu anatuadibisha kwa mafaa yetu kusudi tupate kushirikiana naye katika utakatifu wake.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


Aepuke mabaya, atende mema, atafute amani na kuifuatilia.


Ni nani atakayewazuru ninyi kama mukiwa wenye bidii katika kutenda mema?


Basi kwa kuwa vitu vyote vitaharibiwa namna hii, ninyi munapaswa kuishi maisha matakatifu na kushikamana na ibada,


Lakini muzidi kukomaa katika neema na katika kumujua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Asifiwe, sasa na hata milele! Amina.


Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.


Yefuta akatuma tena wajumbe kwa mufalme wa Amoni


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ