Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 11:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 11:34
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Ahabu alimwelezea muke wake Yezebeli mambo yote Elia aliyofanya na jinsi alivyowaua manabii wa Bali kwa upanga.


Elia akakimbilia katika muji wa Beri-Seba katika jimbo la Yuda, kule alikomwacha mutumishi wake,


Siku moja, wanafunzi wa manabii walimulalamikia Elisha wakisema: “Pahali hapa tunapokaa ni padogo sana kwetu!


Halafu akatuma mujumbe kwenda kumuleta Elisha. Wakati uleule, Elisha alikuwa ndani ya nyumba pamoja na wazee waliomutembelea. Mbele ya kufika kwa mujumbe wa mufalme, Elisha akawaambia wazee: “Yule mwuaji amemutuma mutu kuja kunikata kichwa! Atakapofika hapa, mufunge mulango, wala musimuruhusu aingie. Vilevile bwana wake anamufuata nyuma.”


Nyuma ya Yobu kuwaombea warafiki zake, Yawe akamurudishia Yobu hali yake ya kwanza. Akamupa mara mbili ya yote aliyokuwa nayo pale mbele.


Atakuepusha toka kifo wakati wa njaa, toka mapigo ya upanga wakati wa vita.


Tumeponyoka kama ndege katika mutego; mutego umefyatuka, nasi tukaponyoka.


wewe unayewapa wafalme ushindi, unayemwokoa mutumishi wako Daudi!


Macho yangu yamechoka kwa huzuni; yamefifia kwa kutaabishwa na waadui.


Umewaacha watu watukanyage; tumepitia katika moto na katika maji. Lakini sasa umetuleta kwenye usalama.


Wa pili aliitwa Eliezeri, kwa vile Musa alisema: “Mungu wa baba yangu ndiye aliyenisaidia nisiuawe na mufalme wa Misri.”


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


Lakini Yeremia alikuwa akilindwa na Ahikamu mwana wa Safamu kusudi asitiwe katika mikono ya watu na kuuawa.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Wandugu wapendwa, musishangae kwa kuona mateso makubwa ya kuwajaribu munayopata. Musiyahesabu kuwa kitu kigeni kwenu.


Basi, akawashambulia vikali na kuwaua wengi. Kisha akaenda kuishi katika pango la Etamu lililokuwa chini ya jiwe.


Basi, alimutupia Daudi mukuki mara mbili maana alifikiri: “Nitamubanisha Daudi kwenye ukuta.” Lakini Daudi aliepa mara zote mbili.


Saulo alijaribu kumuchoma Daudi kwa mukuki ule. Lakini Daudi aliepa mukuki wa Saulo na mukuki ukapiga ukuta. Daudi akakimbia na kutoroka.


Daudi alikimbia kutoka Nayoti katika Rama, akaenda mpaka kwa Yonatani, akamwambia: “Nimefanya nini? Kosa langu ni gani? Nimemutendea baba yako zambi gani hata anajaribu kuyaangamiza maisha yangu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ