Muzee akaenda, akaikuta maiti ya mutu wa Mungu katika barabara, simba na punda wake pembeni yake. Yule simba hakuikula maiti wala hakumushambulia punda.
Basi, Mungu alitoa ahadi kwa Abrahamu na uzao wake. Maandiko hayasemi kwamba alitoa ahadi zile kwa “wazao wake” kama vile angeitoa kwa watu wengi. Lakini yanasema kwamba “kwa uzao wako”, maana yake kwa mutu mumoja tu ndiye Kristo.
Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.
Kwa njia ya imani, Abrahamu alimutoa Isaka kama vile sadaka wakati Mungu alipopima imani yake. Abrahamu alikubali kumutoa mwana wake wa pekee, ingawa ni yeye ndiye aliyekuwa amepewa ahadi na Mungu.
Lakini mutu anaweza kusema: “Wewe uko na imani, na mimi niko na matendo.” Mimi nitajibu: “Unionyeshe imani yako pasipo matendo, na mimi nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.”