Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 11:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 11:26
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Afazali mali kidogo ya mutu wa haki kuliko utajiri mwingi wa watu waovu.


Wewe unajua ninavyotukanwa, unajua haya na matusi ninazopata; na waadui zangu wote wewe unawajua.


Wanaokutumainia wasifezeheke kwa sababu yangu, ee Bwana wetu, Yawe wa majeshi; wanaokutafuta, wasizarauliwe kwa sababu yangu, ee Mungu wa Israeli.


Faida mwovu anayopata ni ya uongo, lakini anayetenda mema, hakika atapata faida.


Hakika siku nzuri zitafika na tumaini lako halitakuwa la bure.


Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Yule anayemupokea nabii wa Mungu, kwa sababu ni nabii, atapokea zawadi sawa nabii yule. Vilevile yule anayemupokea mwenye haki, kwa sababu ni mwenye haki, atapokea zawadi sawa yule mwenye haki.


Mufurahi na kushangilia, kwa sababu munawekewa zawadi kubwa mbinguni. Ni hivi walivyowatesa manabii walioishi mbele yenu.


“Mujiangalie musifanye matendo mema mbele ya watu kusudi mujionyeshe kwao. Kwa maana mukifanya hivi hamutapata faida kutoka kwa Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Hivi utabarikiwa, kwa maana watu hawa hawana cha kukulipa. Utalipwa hayo yote wakati wenye haki watakapofufuka.”


Ni vile inavyokuwa, hakuna mumoja wenu atakayeweza kuwa mwanafunzi wangu kama asipoacha vyote anavyokuwa navyo.”


Basi mitume wakatoka katika baraza, wakifurahi sana kwa sababu walistahili kuzarauliwa kwa kuteswa kwa ajili ya Yesu.


Kwa sababu hii ninafurahia uzaifu, matusi, ukosefu, taabu na mateso kwa ajili ya Kristo. Kwa maana wakati ninapokuwa muzaifu, basi ndio wakati ule ninapokuwa na nguvu.


tunahuzunishwa lakini tunafurahi siku zote. Tunaonekana kama wamasikini lakini tunatajirisha watu wengi, hatuna kitu, lakini tunakuwa na vitu vyote.


Ninaomba Mungu aifungue mioyo yenu ipate kuona mwangaza wake. Kwa hiyo mutapata kujua tumaini munalokuwa nalo kutokana na mwito wa Mungu. Vilevile mupate kujua utajiri mukubwa wa urizi anaouwekea watu wake,


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Lakini mambo yote yaliyokuwa ya faida kwangu, sasa kwa ajili ya Kristo, ninayahesabu kama kihombo.


Kwa ngambo moja mulitukanwa na kuteswa waziwazi mbele ya watu. Na kwa ngambo ingine mulishirikiana na wale waliotendewa vibaya.


Basi musikate tumaini, kwa maana litawaletea zawadi kubwa.


Basi pasipo imani, hakuna mutu anayeweza kumupendeza Mungu. Kwa maana mutu anayetaka kumwendea Mungu sherti aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba anawapa zawadi wale wanaomutafuta.


Basi tumwendee mbali na kambi, tukikubali kuzarauliwa kama vile yeye alivyozarauliwa.


Ujumbe wa Sheria uliotangazwa na malaika ulitimizwa, na hata kila mutu aliyekosa kuufuata na kuasi aliazibiwa sawa inavyostahili.


Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alitangulia kushuhudia mateso yatakayomupata Kristo na utukufu utakaokuwa nyuma. Nao walijitolea kusudi wapate kuvumbua wakati gani na kwa njia gani mambo haya yatafanyika.


Ninyi ni wenye heri kama watu wakiwatukana kwa ajili ya Kristo, kwa kuwa Roho wa utukufu, maana yake Roho wa Mungu anakaa ndani yenu.


Ninajua mateso yako na umasikini wako, lakini wewe ni tajiri! Vilevile ninajua jinsi unavyotukanwa na wale wanaojidai kuwa Wayuda lakini si Wayuda; wao ni kikundi cha wenye kuabudu Shetani!


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


Yawe akubariki kwa yote uliyoyafanya. Yawe wa Israeli uliyemukimbilia akulinde chini ya mabawa yake, akupe zawadi kamilifu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ