Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 11:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Lakini kwa hakika walitamani sana inchi inayokuwa bora zaidi, ndiyo inchi ya mbinguni. Kwa sababu hii Mungu hasikii haya kuitwa Mungu wao, maana amewatayarishia muji.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 11:16
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Usiku uleule Yawe alimutokea na kumwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako Abrahamu. Usiogope; niko pamoja nawe. Nitakubariki na kuwazidisha wazao wako kwa ajili ya Abrahamu, mutumishi wangu.”


Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Yawe, Mungu wa babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutuma kwao. Hili ndilo jina langu milele, na hivi ndivyo nitakavyokumbukwa katika vizazi vyote.


Kisha Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Musa akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumwangalia Mungu.


Yawe akamwambia: “Hivyo Waisraeli watapata kuamini kwamba mimi Yawe, Mungu wa baba zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, nimekutokea.”


Kutakuja siku ambazo nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Waisraeli, nao watakuwa watu wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.


Na juu ya kufufuka kwa wafu, hamujasoma katika kitabu cha Sheria ya Musa, yale maandiko yanayosema juu ya kichaka kilichowaka moto? Mungu alimwambia Musa: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’ ”


Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu kati ya watu wa kizazi hiki kisichokuwa na uaminifu mbele ya Mungu na chenye zambi, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile, atakapokuja pamoja na wamalaika watakatifu, akitukuzwa na Baba yake.”


“Musiogope ninyi kundi dogo! Kwa kuwa Baba yenu amependelea kuwapa ninyi ule Ufalme wake.


Musa alionyesha waziwazi kwamba wafu watafufuka. Katika maandiko yake yanayosema juu ya kichaka kilichowaka moto, yeye anamutaja Bwana kuwa ni ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’


Ndani ya nyumba ya Baba yangu kuna nafasi nyingi za kukaa. Isingekuwa hivi singewaambia kwamba ninakwenda kuwatayarishia nafasi.


‘Mimi ni Mungu wa babu zako, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.’ Musa akatetemeka kwa woga wala hakusubutu kuendelea kuangalia.


Lakini sisi ni wenyeji wa mbingu, tunamungojea Mwokozi wetu Bwana Yesu Kristo, afike kutoka kule.


Bwana ataniokoa toka katika mambo yote mabaya na kunipeleka salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Bwana atukuzwe milele na milele. Amina.


Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Kwa maana Abrahamu alitazamia kuona muji wenye musingi wa nguvu, muji ambao Mungu mwenyewe ndiye fundi aliyeuchapa na kuujenga.


Maana watu wanaosema maneno kama haya wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta inchi yao wenyewe.


kwa maana Mungu alikuwa ametayarisha mambo mazuri zaidi kwa ajili yetu kusudi wao wenyewe wasipate kukamilishwa bila sisi vilevile.


Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.


Kwa maana hapa katika dunia hatuna muji unaodumu, lakini tunatazamia muji ule unaokuja.


Yeye anawatakasa watu toka katika zambi, na wale wanaotakaswa naye, wote ni watoto wa Baba mumoja. Ni kwa sababu hiyo Yesu hasikii haya ya kuwaita wandugu zake.


Nikaona muji mutakatifu, ndio Yerusalema mupya, uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu, nao ukitengenezwa vizuri kama vile bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya kwenda kukutana na mume wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ