15 Kama wangekumbuka inchi yao walioiacha zamani, wangeweza kupata namna ya kurudia kule.
Tera akatwaa Abramu mwana wake, Loti mujukuu wake aliyekuwa mwana wa Harani, na Sarai muke wa Abramu, wakaondoka wote pamoja toka Uri, muji wa Wakaldea, na kwenda katika inchi ya Kanana. Lakini walipofika Harani, wakakaa pale.
Wakati ule, njaa ikatokea katika inchi. Njaa hiyo ilikuwa kali, hivyo Abramu akalazimika kwenda Misri kukaa kule kwa muda.
Uniapie kwamba utakwenda mpaka katika inchi yangu, kwa jamaa zangu, umutafutie mwana wangu Isaka muke.”
Alitwaa nyama wake wote pamoja na mali yote aliyopata kule Padani-Aramu, akaanza safari ya kurudi katika inchi ya Kanana kwa baba yake Isaka.
Maana watu wanaosema maneno kama haya wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta inchi yao wenyewe.