Waebrania 11:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Kwa sababu hiyo, kwa njia ya mutu mumoja aliyekuwa akingojea kufa, kukazaliwa wazao wengi sana kama nyota na kama muchanga unaokuwa kandokando ya bahari.
Shauri langu ni kwamba uwakusanye kwako watu wote wa Israeli tangia Dani mpaka Beri-Seba wakuwe wengi kama muchanga wa bahari, na wewe mwenyewe peke yako uende kwa vita.
Mufalme Daudi hakuwahesabu wale waliokuwa chini ya umri wa miaka makumi mbili kwa maana Yawe aliahidi kuwaongeza Waisraeli kuwa wengi kama nyota za mbinguni.
Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.
Maana, hata kama sasa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaorudi. Maangamizi yamepangwa yafanyike, nayo yatafanyika kwa haki tu.
Kama vile nyota katika anga na muchanga katika bahari visivyoweza kuhesabiwa, ndivyo nitakavyoongeza hesabu ya wazao wa mutumishi wangu Daudi na hesabu ya makuhani wa ukoo wa Lawi.
naye atakwenda kuwadanganya watu wa mataifa wanaokuwa katika pande zote za dunia, ndio wanaoitwa Gogi na Magogi. Shetani atawakusanya kwa kupigana vita, nao watakuwa wengi kama vile muchanga wa bahari.
Samweli akajibu: “Yawe ni mushuhuda juu yenu, na mufalme wake muchaguliwa leo ni mushuhuda kuwa mumeniona sina kosa.” Wao wakajibu: “Yeye ni mushuhuda.”