Waebrania 11:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Kwa njia ya imani, Sara mwenyewe vilevile, ijapokuwa alikuwa muzee sana, alijaliwa uwezo wa kupata mimba kwa sababu aliamini kwamba Mungu atatimiza ahadi yake.
Hata Elizabeti wa jamaa yako, amepata mimba, naye atazaa mutoto mwanaume, ijapokuwa yeye ni muzee. Yeye aliyekuwa akiitwa tasa, sasa huu ni mwezi wa sita wa mimba yake.
Maana yake, si wale waliozaliwa sawa na kawaida wanaohesabiwa kuwa watoto wa Mungu; lakini ni wale waliozaliwa kufuatana na ahadi ya Mungu ndio wanaohesabiwa kuwa wazao wake wa kweli.