Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 10:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Kwa ngambo moja mulitukanwa na kuteswa waziwazi mbele ya watu. Na kwa ngambo ingine mulishirikiana na wale waliotendewa vibaya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 10:33
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nimekuwa mugeni kwa wandugu zangu, kaka na dada zangu hawanitambui.


Kwa wengi nimekuwa mushangao, lakini wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.


Ee Mungu, simama sasa ujitetee! Ukumbuke mazarau ya kila siku ya wasiokujua.


Ee Bwana, uwalipize mataifa jirani mara saba kwa ajili ya matusi waliyokutukana.


Ee Bwana, ukumbuke matusi ya mutumishi wako, jinsi ninavyovumilia mazarau ya mataifa.


Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Nitakutupia uchafu, na kukuzaraulisha, na kukufanya kuwa mushangao kwa watu.


Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.


Kwa maana inaonekana kuwa Mungu ametufanya sisi mitume kuwa watu wenye hali ya chini kabisa. Tunahesabiwa kama watu wanaohukumiwa kufa mbele ya watu. Tumewekwa kama kitu cha kushangaza, kinachoangaliwa na dunia nzima, nao wamalaika na watu vilevile.


Kwa sababu hii ninafurahia uzaifu, matusi, ukosefu, taabu na mateso kwa ajili ya Kristo. Kwa maana wakati ninapokuwa muzaifu, basi ndio wakati ule ninapokuwa na nguvu.


Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.


Lakini, mumefanya vizuri kwa kushirikiana pamoja nami katika taabu yangu.


Wandugu, mambo yale yale yaliyotokea makanisa ya Mungu ya Yudea yanayoungana na Yesu Kristo, ndiyo yaliyowatokea ninyi vilevile. Kwa maana ninyi muliteswa na wanainchi wenzenu kama vile wao walivyoteswa na wanainchi wenzao Wayuda.


Basi, usisikie haya ya kutoa ushuhuda kwa ajili ya Bwana wetu, wala usisikie haya kwa sababu yangu mimi ninayekuwa katika kifungo kwa ajili yake. Lakini ushiriki nami katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kufuatana na uwezo unaopewa na Mungu.


Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake.


Wengine walichekelewa na kupigwa fimbo, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa katika kifungo.


Kwa maana katika vita munayofanya kwa kushinda zambi, hamujapigana bado mpaka kufa.


Basi tumwendee mbali na kambi, tukikubali kuzarauliwa kama vile yeye alivyozarauliwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ