Waebrania 10:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
25 Tusiache kukusanyika pamoja, kama vile wamoja wanavyozoea kufanya. Lakini tuonyane, na zaidi sana kufuatana na vile munavyoona kwamba Siku ya Bwana inakaribia.
Siku moja tulipokuwa tukienda kule kwenye nafasi ya kufanyia maombi, tukakutana na mujakazi mumoja. Yule mwanamuke alikuwa na pepo wa kuaguza ndani yake. Na kwa njia ya uaguzi ule aliwatajirisha wabwana wake.
Siku ya kwanza ya juma, tulikuwa tunakusanyika kwa kumega mukate. Paulo akasemezana na watu na kuendelea kuwahubiria mpaka katikati ya usiku, kwa sababu alikusudia kuondoka kesho yake.
Aliyepewa zawadi ya kuonya wengine, awaonye. Aliyepewa zawadi ya kutoa, atoe kwa moyo mweupe. Anayesimamia wengine, awasimamie kwa bidii. Aliyepewa zawadi ya kuhurumia wengine, afanye vile kwa furaha.
Basi kama kanisa zima limekusanyika, na watu wote wanaanza kusema kwa luga za ajabu; na kisha watu wasioelewa kitu au wasioamini wakiingia katika mukutano wenu hawatasema kuwa ninyi ni wenda-wazimu?
Lakini hali ya kazi ya kila mutu itaonekana wazi, kwa sababu Siku ile ya hukumu itaionyesha waziwazi. Kwa maana Siku ile itajitokeza katikati ya moto, na moto ule ndio utakaopima na kuonyesha hali ya kazi ya kila mutu.
Lakini muonyane kila siku kwa muda wote ambao lile neno “leo” linalotajwa lingali linatuelekea kusudi hata mumoja wenu asikuwe mugumu kwa kudanganywa na zambi.
Bwana hakawii kutimiza ahadi zake kama vile watu wamoja wanavyozania. Yeye anavumilia kwa ajili yenu, maana hapendi hata mutu mumoja apotee, lakini anataka watu wote wageuke toka zambi zao.