Majaribu yale munayopata, ni yale yanayowapata watu wengine wote. Mungu hatawaachilia kujaribiwa kupita nguvu zenu, kwa maana yeye ni mwaminifu. Jaribu litakapowatokea, atawapatia nguvu ya kulivumilia, hata muweze kulishinda.
Kufuatana na ushuhuda wa kazi hii, watu watamutukuza Mungu kwa kuona jinsi munavyoonyesha utii wenu katika kushika Habari Njema ya Kristo. Vilevile wanamutukuza kwa kuona moyo wa kutoa munaokuwa nao katika kushirikiana mali yenu pamoja nao na sisi.
Kwa njia ya imani, Sara mwenyewe vilevile, ijapokuwa alikuwa muzee sana, alijaliwa uwezo wa kupata mimba kwa sababu aliamini kwamba Mungu atatimiza ahadi yake.
Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.
Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.
Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.
Lakini inafaa aombe kwa imani pasipo kuwa na mashaka. Kwa maana mutu anayekuwa na mashaka anafanana na zoruba katika bahari inayosukumwa na upepo na kutupa maji huku na huko.