Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sheria ya Kiyuda ni mufano wa mema yatakayotokea, lakini si kitambulisho kinachoonyesha mambo yale kamili. Kwa sababu hii Sheria haiwezi hata mara moja, kwa njia ya sadaka zinazotolewa mara nyingi kila mwaka, kuwafanya wakamilifu wale wanaomwendea Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 10:1
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha akaleta mbele ile sadaka ya kuteketezwa akatolea sadaka hiyo kulingana na agizo.


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Mambo hayo yote ni kivuli cha mambo yatakayokuja, lakini ukweli wa mambo yote ni Kristo mwenyewe.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Ukuhani ndio ulikuwa musingi wa Sheria iliyotolewa kwa Waisraeli. Basi ikiwa ukamilifu ulipatikana kwa njia ya kazi ya ukuhani wa uzao wa Lawi, hakungekuwa tena lazima kutokee kuhani mwingine anayekuwa sawa na Melkisedeki, kwa pahali pa kuhani anayekuwa sawa na Haruni.


Kazi wale makuhani wanayofanya ni mufano na kitambulisho kinachoonyesha jinsi mambo kamili yanavyopitika mbinguni. Maneno hayo yanalingana na yale yaliyomutokea Musa. Wakati Musa alipokuwa karibu ya kujenga Hema, Mungu alimwambia: “Ufanye angalisho kusudi upate kutengeneza kila kitu kufuatana na mufano niliokuonyesha kwa mulima.”


Lakini Kristo alikuja kuwa Kuhani Mukubwa anayeshugulika na mambo mema ambayo sasa yamekwisha kutokea. Yeye alipita katika hema inayokuwa bora zaidi na kamilifu. Hema hii haikutengenezwa na watu, maana yake si ya dunia hii.


Basi ilikuwa lazima vitu vile vinavyoonyesha mufano wa mambo yanayopitika katika mbingu vitakaswe kwa njia ile. Lakini mambo kamili ya mbinguni yanahitaji kutakaswa kwa sadaka inayokuwa bora zaidi.


Kuhani Mukubwa wa Wayuda anaingia katika Pahali Patakatifu Sana kila mwaka, akibeba damu ya nyama. Lakini Kristo hakuingia humo kusudi ajitoe mwenyewe sadaka mara nyingi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ