Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 1:2
70 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo akawaita wana wake, akasema: “Mukusanyike pamoja niwaambie mambo yatakayowapata siku zinazokuja.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Yawe, Mukombozi wako, aliyekuumba tangu katika tumbo, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe niliyeumba vitu vyote. Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu, niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!


Ni mimi niliyeifanya dunia, na kuumba mwanadamu anayeishi humo. Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu, na kundi lote la nyota liko kwa amri yangu.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Hasira ya Yawe haitatulia, mpaka atakapotimiza na kukamilisha mapenzi ya moyo wake. Kutakuja siku ambazo mutaelewa vema mambo hayo.


Lakini katika siku zinazokuja nitawarudisha tena Moabu katika hali yao. –Ni ujumbe wa Yawe. Hii ndiyo hukumu juu ya Moabu.


Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.


nami nimekuja kukusaidia upate kuyafahamu mambo yatakayowapata watu wako wakati unaokuja, maana maono uliyoona yanaelekea wakati unaokuja.


Lakini, kuna Mungu mbinguni ambaye anafumbua mafumbo, naye amekujulisha, ee mufalme Nebukadneza, mambo yatakayotukia katika siku zinazokuja. Ndoto yako na maono yaliyokufikia ulipokuwa unalala ni haya:


Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.


Kutakuja wakati ambapo mulima wa nyumba ya Yawe utakuwa mukubwa kuliko milima yote. Utanyanyuliwa juu ya vilima vyote. Watu wengi watakimbilia kule,


Sasa ninarudi kwa watu wangu, lakini mbele sijaondoka, acha nikuambie mambo ambayo watu hao watawatendea watu wako siku zinazokuja.


Adui aliyepanda nyasi ni Shetani. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni wamalaika.


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Lakini wakati walimaji walipomwona yule mwana, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue, na shamba hili litakuwa urizi wetu!’


Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani Mukubwa akamwambia: “Ninakuapisha kwa jina la Mungu Mwenye Uzima, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Huu ndio mwanzo wa Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.


Mwenye shamba alibaki tu na mutu mumoja, naye alikuwa mwana wake mupendwa. Mwisho akamutuma kwao, akisema: ‘Ninajua kwamba watamuheshimu mwana wangu.’


Lakini wale walimaji walipomwona akikuja, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue, na shamba hili litakuwa urizi wetu!’


Neno alikuwa yuko katika dunia, nayo dunia iliumbwa kwa njia yake, lakini ijapokuwa vile haikumutambua.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, wala hakuna hata kitu kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.


Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.


Na ikiwa Mungu ametukuzwa kwa njia yake, basi Mungu vilevile atamutukuza Mwana kwa njia yake mwenyewe, naye atamutukuza bila kukawia.


Siwaiti ninyi tena watumishi, kwa sababu mutumishi hajui mambo bwana wake anayofanya. Ninawaita ninyi warafiki kwa sababu nimewajulisha yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.


Yote Baba anayokuwa nayo ni yangu. Ni kwa sababu hii nilisema kwamba maneno Roho atakayowaambia yatatokana na yale yanayokuwa ndani yangu.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Kulitokea mabishano kati ya wanafunzi wa Yoane na Muyuda mumoja juu ya desturi zao za kujitakasa.


Kama vile Baba ana uwezo wa kupana uzima, ndivyo vilevile amemupa Mwana uwezo wa kupana uzima.


Vilevile amemupa Mwana mamlaka ya kuhukumu, kwa sababu yeye ni Mwana wa Mutu.


Tunajua kwamba Mungu alisema na Musa, lakini hatujui pahali mutu yule anapotoka!”


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


‘Mungu anasema: Katika siku za mwisho, nitashusha Roho wangu juu ya watu wote; wana wenu na wabinti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono nao wazee wenu wataota ndoto.


Na kama sisi ni watoto, basi tutakuwa na sehemu katika urizi ule Mungu aliowaahidi watu wake, na tutashiriki pamoja na Kristo katika urizi ule; kwa maana kama tukiteswa pamoja naye tutatukuzwa pamoja naye vilevile.


Ninatangaza hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichwa kwa watu, na iliyopangwa na Mungu mbele ya kuumbwa kwa dunia kwa ajili ya utukufu wetu.


Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Kusudi la mupango ule utakaotimia kwa wakati uliowekwa, ni kukusanya viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia chini ya utawala wa Kristo.


Na hivi nipate kuwaelezea vema namna unavyotimia ule mupango uliokuwa umefichwa tangu zamani na Mungu, muumbaji wa vitu vyote.


“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.


Maana ninajua kwamba nyuma ya kifo changu hakika mutakuwa waovu na kuacha ile njia niliyowaamuru muifuate. Na katika siku zinazokuja mutapatwa na hasara kwa sababu mutafanya maovu mbele ya Yawe na kumukasirikisha kwa matendo yenu.”


Mambo haya yote yatakapowapata huko, kisha mukipata taabu, mutamurudilia Yawe na kumutii.


Kwa maana Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi: “Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.” Wala hakusema maneno haya juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwana wangu.”


Lakini juu ya Mwana, Mungu alisema: “Kiti chako cha kifalme, Ee Mungu, kitadumu hata milele. Unatawala ufalme wako kwa haki.


Kwa njia ya imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa amri ya Mungu, hata vitu vinavyoonekana, viliumbwa kutoka vile visivyoonekana.


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.


Basi, kwa kuwa tuko na Kuhani Mukubwa zaidi aliyeingia mbinguni, ndiye Yesu Mwana wa Mungu, tushikamane sana na imani tunayotangaza.


Ijapokuwa alikuwa Mwana wa Mungu, alijifunza kutii kwa njia ya mateso yale aliyopata.


Sheria ya Musa inawaweka watu wenye uzaifu kuwa Makuhani Wakubwa, lakini kufuatana na kiapo kilichokuja nyuma ya Sheria ile, Mwana anayekuwa mukamilifu kwa milele aliwekwa kuwa Kuhani Mukubwa.


Hakuna mambo yaliyoandikwa juu ya baba ya Melkisedeki, wala mama yake, wala majina ya babu zake. Tena, habari za kuzaliwa kwake na za kufa kwake hazijulikani. Anafanana na Mwana wa Mungu kwa kuwa yeye ni kuhani kwa milele.


Ingekuwa hivi, ingemupasa ateswe mara nyingi tangu kuumbwa kwa dunia. Lakini sasa, wakati ukikaribia kwa mwisho, yeye alitokea mara moja tu kusudi awasamehe watu zambi kwa njia ya kujitoa mwenyewe sadaka.


Yeye ndiye aliyechaguliwa na Mungu mbele ya kuumbwa kwa dunia, na alifunuliwa kwa ajili yenu katika nyakati hizi za mwisho.


Mbele ya yote, mujue kwamba katika siku za mwisho kutakuja watu watakaoishi kufuatana na tamaa zao wenyewe. Watawachekelea ninyi


Wao waliwaambia: “Katika siku za mwisho, kutakuja watu watakaowachekelea, wakiishi kwa kufuata tamaa zao mbaya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ