Waebrania 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu, mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”
Daudi yeye mwenyewe, akiongozwa na Roho Mutakatifu, alisema: ‘Bwana wetu Mungu alimwambia Bwana wangu: Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu, mpaka nitakapoweka waadui zako chini ya miguu yako.’
Lakini Stefano akijazwa na Roho Mutakatifu, akakaza macho kuelekea mbingu akaona mwangaza wa utukufu wa Mungu naye Yesu akisimama na mamlaka karibu na Mungu.
Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.
Wafalme hao walipoletwa, Yoshua akawaita Waisraeli wote na wakubwa wa waaskari waliokwenda naye kwa vita, akawaambia: “Mukuje karibu muwakanyage wafalme hawa kwenye shingo yao.” Nao wakasogea na kuwakanyaga kwenye shingo.