3 Wandugu za mama yake wakatangaza maneno popote kule Sekemu kwa jina lake, na watu wote wa Sekemu wakaamua kumufuata maana alikuwa ndugu yao.
Siku moja Labani akamwambia Yakobo: “Wewe ni jamaa yangu lakini hiyo haisemi kwamba utanitumikia bure. Uniambie unataka mushahara gani!”
Mujumbe mumoja akamwendea Daudi na kumwambia: “Watu wa Israeli wamevutwa na Abusaloma!”
Mwovu anajisifia tamaa zake mbaya, anapata faida kwa njia mbaya, anazarau na kumukataa Yawe.