Hamutahitaji kupigana vita hivi. Ninyi mujipange tu halafu mungojee, na mutaona Yawe akiwashinda kwa jina lenu. Enyi watu wa Yuda na Yerusalema, musiogope wala musifazaike. Muende kwa vita, naye Yawe atakuwa pamoja nanyi!”
Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.
Wale watu wenye elimu walipokwisha kwenda, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto na kumwambia: “Amuka, utwae mutoto pamoja na mama yake na mukimbilie Misri. Mukae kule mpaka nitakapokuambia kwamba urudie, kwa maana Herode anamutafuta mutoto kusudi amwue.”
Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hao, maana kesho, wakati kama huu, nitawaangamiza wote kwa kuwatia katika mikono ya Waisraeli; nanyi mutakata mishipa ya miguu ya farasi wao na kuteketeza magari yao kwa moto.”
Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni alikuwa na kazi ya kutumika mbele yake. Waisraeli wakamwuliza Yawe: “Twende tena kupigana na wandugu zetu, watu wa kabila la Benjamina?” Yawe akawaambia: “Muende. Kesho nitawatia katika mikono yenu.”
Basi, roho wa Yawe akamujaza Otinieli, naye akakuwa mwamuzi wa Waisraeli. Otinieli alikwenda katika vita naye Yawe akamutia Kusani, Yule-Mwovu-Sana, ufalme wa Mesopotamia, katika mikono yake.
Akawaambia: “Munifuate, maana Yawe amewatia waadui zenu Wamoabu katika mikono yenu.” Wakamufuata mpaka kwenye kivuko cha Yordani na kukiteka toka katika mikono ya Wamoabu, wakazuia mutu yeyote kupita.
Basi, Gideoni akatwaa vyakula vya wale waliokuwa wanaondoka na baragumu, akawaaga waende kwao. Yeye akabaki na wale watu mia tatu. Kambi ya Wamidiani ilikuwa katika bonde upande wao wa chini.