Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 7:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Basi, Gideoni akatwaa vyakula vya wale waliokuwa wanaondoka na baragumu, akawaaga waende kwao. Yeye akabaki na wale watu mia tatu. Kambi ya Wamidiani ilikuwa katika bonde upande wao wa chini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 7:8
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku hiyo, baragumu kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea katika inchi ya Asuria au waliotawanywa katika inchi ya Misri watarudi na kumwabudu Yawe juu ya mulima mutakatifu kule Yerusalema.


Uwaambie watu wa Israeli hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa saba mutafanya siku ya mapumziko, siku ya ukumbusho itakayotangazwa kwa mulio wa baragumu na kufanya mukutano mutakatifu.


Kisha, katika siku ya kumi ya mwezi wa saba ambayo ni siku ya kufanyiwa upatanisho mutatuma mutu kupiga baragumu katika inchi yote.


Wakati wa vita katika inchi yenu juu ya waadui wanaowashambulia, mutatoa kitambulisho cha vita kwa kupiga baragumu hizi kusudi Yawe, Mungu wenu apate kuwakumbuka na kuwaokoa na waadui zenu.


kwa rafla, kama vile mutu anavyofunga jicho na kulifungua, wakati ngunga ya mwisho itakapolia. Kwa maana wakati itakapolia, wafu watafufuka na kupata kuwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi wote tutabadilishwa.


Basi, watu wakapiga kelele nayo mabaragumu yakiwa yanapigwa. Watu waliposikia sauti ya mabaragumu walipiga kelele kubwa, na kuta za muji zikaanguka chini kabisa. Mara tu watu wakaushambulia muji, kila mumoja kutoka pahali aliposimama, wakauteka.


Makuhani saba, kila mumoja akiwa anabeba baragumu yake ya pembe ya kondoo dume, watatangulia mbele ya Sanduku la Agano. Katika siku ya saba mutauzunguka muji ule mara saba, nao makuhani wakipiga mabaragumu.


Alipofika kule akapiga baragumu katika inchi ya milima ya Efuraimu, nao Waisraeli wakateremuka pamoja naye kutoka kule kwenye milima naye akawatangulia.


Wamidiani, Waamaleki na watu wote wanaokaa pembeni ya muto Yordani wakapiga kambi zao katika bonde la Yezereheli.


Yawe akamwambia Gideoni: “Kwa hao watu mia tatu waliokunywa kwa kulamba kama imbwa, nitawaokoa Waisraeli na kuwatia Wamidiani katika mikono yao. Lakini wale wengine wote warudie kwao.”


Usiku ule, Yawe akamwambia Gideoni: “Kwenda uwashambulie katika kambi yao, maana nimewatia katika mikono yako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ