Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe akamwambia Gideoni: “Watu unaokuwa nao ni wengi sana kwangu mimi kwa kuwatia Wamidiani katika mikono yao. Waisraeli wasipate kujisifu mbele yangu na kusema kwamba wamejiokoa kwa nguvu zao wenyewe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 7:2
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”


Yawe akawashinda Waetiopia mbele ya Asa na jeshi lake la watu wa Yuda. Waetiopia wakakimbia.


Maana mufalme wa Asuria alisema: Kwa nguvu zangu mwenyewe nimetenda hayo, na kwa hekima yangu, maana mimi ni mwerevu! Nimeondoa mipaka kati ya mataifa, nikanyanganya akiba zao; kama ngombe dume nimewaporomosha walioikaa juu ya viti vya kifalme.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Kiburi cha wanadamu kitashushwa, majivuno ya watu yatanyenyekezwa, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ulikuwa na kiburi kwa sababu ya uzuri wako. Uliharibu hekima yako kwa sababu ya utukufu wako. Nilikutupa chini kwenye udongo, nikakufanya kuwa kitisho kwa wafalme.


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Kwa hiyo, wanazitambikia nyavu zao, na kuzifukizia ubani; maana kwa njia ya vitu hivyo mapato yao yanaongezeka, na wanakuwa na chakula kingi.


Nami Yawe nitasaidia kwanza jamaa za Yuda kusudi wazao wa Daudi na wakaaji wa Yerusalema wasijione kuwa wenye utukufu zaidi kuliko watu wengine wa kabila la Yuda.


Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.


Kutoka kila kabila la Israeli, mutapeleka watu elfu moja kwa vita.


Basi musizarau yale matawi yaliyokatwa. Ninyi hamuna cha kujivunia, kwa maana si ninyi munaoshikilia shina, lakini ni shina linalowashikilia.


Basi sasa mutu ataweza kujivuna? Hapana! Kwa sababu gani? Kwa sababu anatii Sheria? Hapana. Lakini kwa sababu anamwamini Yesu.


Lakini sisi tunaokuwa na hazina hii ya kiroho, tuko vyombo vya udongo, kusudi watu waone waziwazi uwezo huu wa ajabu sana unaotoka kwa Mungu lakini si kwetu sisi wenyewe.


Si kwa matendo yenu, kusudi mutu asipate kujivuna.


isipokuwa tu kwa sababu ya majivuno ya waadui zao, kusudi waadui zao wasifikiri kwamba wamepata kuwaangamiza, nami Yawe sikufanya kitu katika mambo haya!


Hivyo mufanye angalisho kusudi musijisemeshe ndani ya mioyo yenu: ‘Tumejitajirisha kwa uwezo na nguvu zetu wenyewe’.


Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye anayewapa uwezo wa kupata utajiri. Anafanya hivyo kwa kuimarisha agano alilofanya na babu zenu mpaka leo.


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ