Halafu watu wakafurahi kwa sababu walitoa kwa mapenzi yao, maana kwa moyo wao wote walimutolea Yawe kwa mapenzi yao, naye mufalme Daudi akafurahi sana.
Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.
Ni hivi niliona kuwa ni vizuri kuwashauri wandugu hawa watangulie kufika kwenu mbele yangu kusudi watayarishe vile vitu mulivyoahidi kutoa kwa mapenzi yenu. Hivi vitakuwa tayari na itaonyesha kwamba mumevitoa kwa moyo mwema, wala si kwa uchoyo.