Tumekuwa kama watu ambao haujawatawala hata kidogo, kama watu ambao hawakujulikana kwa jina lako. Heri ungepasua mbingu ushuke chini, milima ingetetemeka mbele yako!
Yawe alikuja kutoka mulima Sinai, alitutokea kutoka mulima Seiri, aliangaza kutoka mulima Parani. Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika, na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.
Katika wakati ule sauti yake ilitetemesha dunia, lakini sasa ametuahidi hivi: “Nitatetemesha dunia mara moja tena, wala si dunia tu, lakini mbingu vilevile.”