Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mimi nitamuchochea Sisera, jemadari wa waaskari wa mufalme Asikie, akuje na waaskari na magari yake kupigana nawe kwenye muto Kisoni, na kumutia katika mikono yako.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 4:7
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Elia akawaambia: “Muwakamate manabii wote wa Bali. Musimwache hata mumoja wao atoroke!” Basi, watu wakawakamata wote, naye Elia akawapeleka kwenye muto Kisoni, akawauia kule.


Mimi nitafanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu, nao watawafuatilia katikati ya bahari. Nami nitajipatia utukufu kutokana na kuangamizwa kwa mufalme wa Misri na jeshi lake, magari yake ya vita pamoja na wapanda-farasi wake.


Halafu mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye atawafuatilia. Nami nitajipatia utukufu kwa kumwangamiza yeye na jeshi lake. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.” Basi, Waisraeli wakafanya hivyo.


Yawe akafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye akawafuatilia Waisraeli ambao walikuwa wameondoka Misri katika uhuru.


Lakini kama hakukuwa amemuvizia, lakini ni kwa musiba, basi, yule mwuaji ataweza kukimbilia usalama pahali nitakapowachagulia.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hata kidogo maana nimewatia katika mikono yako, wala hakuna hata mumoja atakayeweza kukushinda.”


Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hao, maana kesho, wakati kama huu, nitawaangamiza wote kwa kuwatia katika mikono ya Waisraeli; nanyi mutakata mishipa ya miguu ya farasi wao na kuteketeza magari yao kwa moto.”


Hapo, ninyi mutatokea kutoka kule mulikokuwa munavizia na kuuteka muji, maana Yawe, Mungu wenu, atautia muji huo katika mikono yenu.


Debora akamwambia Baraka: “Simama! Leo ni siku ambayo Yawe atamutia Sisera katika mikono yako. Yawe anakwenda mbele yako.” Basi, Baraka akashuka kutoka kwenye mulima Tabori akiwaongoza watu wake elfu kumi.


Baraka akamwambia Debora: “Kama utakwenda pamoja nami, nitakwenda. Lakini usipokwenda pamoja nami, sitakwenda.”


Mafuriko ya muto Kisoni yaliwapeleka mbali, mafuriko makali ya muto Kisoni. Songa mbele kwa nguvu, ee nafsi yangu!


Kisha akamwambia: “Kwa nini unawasikiliza watu wanaokuambia: ‘Daudi anataka kukuzuru’?


Kisha akamwambia Daudi: “Wewe una haki kuliko mimi; umenilipa mazuri, wakati mimi nimekulipa mabaya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ