Mutakwenda kwa kupapasapapasa muchana kama vipofu wala hamutafanikiwa katika shuguli zenu. Mutakuwa munateswa kila mara na hakutakuwa mutu wa kuwasaidia.
Nao wakamujibu: “Ni kweli kwamba inchi hii ya milima haitutoshi. Hata hivyo wale Wakanana wote wanaokaa kwenye bonde wana magari ya chuma, vilevile wale wote wanaokaa Beti-Seani pamoja na vijiji vyake, na wale wanaoishi katika Bonde la Yezereheli.”
Yawe alikuwa pamoja na watu wa kabila la Yuda, nao wakaiteka inchi ya milima. Lakini hawakuweza kuwashinda wenyeji wa inchi ya bonde kwa sababu magari yao ya vita yalikuwa ya chuma.
Lakini Waisraeli walipomulilia Yawe, basi, aliwapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Ehudu, mwana wa Gera wa kabila la Benjamina. Alikuwa mwenye kutumikisha zaidi mukono wa kushoto. Waisraeli wakamutuma apeleke zawadi zao kwa Mwana-Ngombe, mufalme wa Moabu.