Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe akawatia katika mikono ya mufalme wa Kanana, jina lake Asikie, ambaye aliishi Hazori. Jemadari wa waaskari wake aliitwa Sisera, mukaaji wa Haroseti-Hagoimu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 4:2
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata Waasuria wameshirikiana nao, wamewaunga mukono wazao wa Loti!


Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.


Na kwa kuona mutumishi yule hakukuwa na jinsi ya kulipa deni lile, bwana wake akaamuru auzishwe kuwa mutumwa, yeye na muke wake pamoja na watoto wake na vyote alivyokuwa navyo viuzishwe vilevile, kusudi apate kumulipa.


Mufalme Yabini wa muji wa Hazori alipopata habari hizo, alipeleka ujumbe kwa mufalme Yobabu wa Madoni, kwa mufalme wa Simuroni na mufalme wa Akisafu,


Hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli, naye akawatia katika mikono ya Wafilistini na Waamoni.


akakusanya waaskari wake wote na magari yake mia tisa ya chuma, akaondoka Haroseti-Hagoimu, akaenda kwenye muto Kisoni.


Baraka akawafuatilia waaskari wale na magari mpaka Haroseti-Hagoimu na kuwaua waaskari wote wa Sisera kwa mapanga. Hakukubaki hata mutu mumoja.


Lakini wao walimusahau Yawe, Mungu wao, naye akawatia katika mikono ya Sisera, jemadari wa waaskari wa muji wa Hazori, na katika mikono ya Wafilistini na katika mikono ya mufalme wa Moabu. Mataifa hayo yalipigana na babu zenu na kuwashinda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ