Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.
Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.
Waisraeli walitenda tena uovu mbele ya Yawe. Yawe akamutia nguvu mufalme wa Moabu aliyeitwa Mwana-Ngombe kusudi awashambulie Waisraeli, kwa sababu walitenda uovu mbele ya Yawe.