Hivyo, ukawatia katika mikono ya waadui zao, nao wakawatesa. Lakini wakiwa katika mateso yao, wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa rehema zako nyingi, ukawatumia viongozi wa kuwaokoa; nao wakawakomboa toka katika mikono yao.
Kila mara Yawe alipowapelekea mwamuzi, yeye mwenyewe alikuwa pamoja na mwamuzi yule, akawaokoa toka katika mikono ya waadui zao muda wote wa maisha ya mwamuzi yule. Ingawa hivyo, Yawe aliwaonea huruma aliposikia kilio chao kutokana na mateso na masumbuko yao.
Lakini Waisraeli walipomulilia Yawe, basi, aliwapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Ehudu, mwana wa Gera wa kabila la Benjamina. Alikuwa mwenye kutumikisha zaidi mukono wa kushoto. Waisraeli wakamutuma apeleke zawadi zao kwa Mwana-Ngombe, mufalme wa Moabu.
Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya mufalme wa Mesopotamia, jina lake Kusani, Yule-Mwovu-Sana. Wakamutumikia kwa muda wa miaka minane.
Babu zenu wakamulilia Yawe, wakisema: ‘Tumefanya zambi kwa sababu tumekuacha wewe Yawe, kwa kutumikia sanamu za mungu Bali na Astaroti. Utuokoe kutoka katika mikono ya waadui zetu, nasi tutakutumikia’.