Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Waisraeli wakamulilia Yawe, naye akawapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Otinieli mwana wa Kenazi, ndugu mudogo wa Kalebu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 3:9
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivyo, ukawatia katika mikono ya waadui zao, nao wakawatesa. Lakini wakiwa katika mateso yao, wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa rehema zako nyingi, ukawatumia viongozi wa kuwaokoa; nao wakawakomboa toka katika mikono yao.


Babu zetu walikutegemea; walikutegemea, nawe ukawaokoa.


Kila mara alipowaua, waliobaki walimugeukia; wakageuka toka ubaya wao, wakamugeukia Mungu kwa moyo.


Basi, Otinieli mwana wa Kenazi, ndugu ya Kalebu, akauteka muji huo, naye Kalebu akamupa binti yake.


Basi, Otinieli mwana wa Kenazi na mudogo wa Kalebu, akauteka, naye Kalebu akamutoa binti yake Akisa aolewe na Otinieli.


Basi wakamulilia Yawe, wakisema: “Tumetenda zambi mbele yako, maana tumekuacha wewe Mungu wetu, tukatumikia Mabali.”


Halafu Yawe akawapa waamuzi ambao waliwaokoa toka katika mikono ya watu walionyanganya mali zao.


Kila mara Yawe alipowapelekea mwamuzi, yeye mwenyewe alikuwa pamoja na mwamuzi yule, akawaokoa toka katika mikono ya waadui zao muda wote wa maisha ya mwamuzi yule. Ingawa hivyo, Yawe aliwaonea huruma aliposikia kilio chao kutokana na mateso na masumbuko yao.


Lakini Waisraeli walipomulilia Yawe, basi, aliwapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Ehudu, mwana wa Gera wa kabila la Benjamina. Alikuwa mwenye kutumikisha zaidi mukono wa kushoto. Waisraeli wakamutuma apeleke zawadi zao kwa Mwana-Ngombe, mufalme wa Moabu.


Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya mufalme wa Mesopotamia, jina lake Kusani, Yule-Mwovu-Sana. Wakamutumikia kwa muda wa miaka minane.


Mufalme Asikie alikuwa na magari ya vita mia tisa ya chuma. Aliwagandamiza sana Waisraeli kwa miaka makumi mbili; nao wakamulilia Yawe awasaidie.


Waisraeli walipomulilia Yawe awaondolee taabu walizopata kwa Wamidiani,


Babu zenu wakamulilia Yawe, wakisema: ‘Tumefanya zambi kwa sababu tumekuacha wewe Yawe, kwa kutumikia sanamu za mungu Bali na Astaroti. Utuokoe kutoka katika mikono ya waadui zetu, nasi tutakutumikia’.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ