Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe aliyaacha kwa kuwajaribu Waisraeli ambao walikuwa hawajapigana vita katika inchi ya Kanana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 3:1
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.


Yawe, Mungu wenu, atafukuza mataifa haya kadiri munavyosonga mbele kidogokidogo. Hamutaweza kuyaangamiza yote kwa mara moja, kwa sababu mukifanya hivyo hesabu ya nyama wa pori itazidi na kuwa kitisho kwenu.


Yeremia, wewe nimekuweka kuwa muchunguzi na mupimaji wa watu wangu, kusudi uchunguze na kuzijua njia zao.


Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunipima nitatoka mule safi kama zahabu.


Kisha watu wote wa kizazi chake wakakufa, kizazi kingine kikafuata ambacho hakikumujua Yawe wala matendo aliyowatendea watu wa Israeli.


Tena ni yeye aliyewakulisha mana katika jangwa, chakula ambacho babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hayo yote kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kwa kuwapima apate kuwajalia mema kwa mwisho.


Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Wandugu wapendwa, musishangae kwa kuona mateso makubwa ya kuwajaribu munayopata. Musiyahesabu kuwa kitu kigeni kwenu.


Majaribu hayo ni kwa ajili ya kupima imani yenu. Zahabu ni kitu kinachoharibika, lakini ingawa vile inapimwa kwa njia ya kuchomwa ndani ya moto. Hivi vilevile imani yenu inayokuwa ya bei kali kuliko zahabu, inapaswa kupimwa kusudi ijulikane kuwa ya kweli. Na kwa sababu hii mutapata sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atakapotokea.


Lakini Yesu hakuwaaminia kwa sababu aliwajua wote vizuri.


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


na hata wakati ambapo wajumbe wa wakubwa wa Babeli waliotumwa kwake kuuliza juu ya mambo ya ajabu yaliyotokea mule, Mungu, alimwacha ajiamulie mwenyewe, kusudi amupime na kujua yote yaliyokuwa ndani ya moyo wake.


Halafu Musa akamulilia Yawe, naye akamwonyesha kipande cha muti, na Musa akakitumbukiza katika maji. Maji hayo yakakuwa mazuri. Kule Mungu aliwapa Waisraeli sharti na agizo, kusudi awapime,


Nyuma ya kifo cha Yoshua, Waisraeli walimwuliza Yawe: “Ni kabila gani litakwenda kupigana kwanza na Wakanana?”


Basi, Yawe akayaacha mataifa hayo ambayo hakumupa Yoshua ushindi juu yao, wala hakuyafukuza mara moja.


Alifanya hivyo kusudi awape watu wa vizazi hivyo ujuzi wa kupigana maana hawakukuwa wameona vita.


pamoja na wazao wao ambao Waisraeli hawakuweza kuwaangamiza kabisa, Solomono aliwatumikisha kazi za kulazimishwa hata leo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ