Musiwaruhusu waishi katika inchi yenu wasiwasukume kutenda zambi mbele yangu. Maana kama mukitumikia miungu yao, hakika ile itakuwa mutego wa kuwanasa.
Lakini kama musipowafukuza wenyeji wa inchi hiyo kwanza, basi wale mutakaowaacha watakuwa kama vile sindano ndani ya macho yenu au miiba kila upande, na watawasumbua.
Muangamize taifa lolote ambalo Yawe, Mungu wenu atalitia katika mikono yenu, wala musilionee huruma. Musiabudu miungu yao, maana jambo hili litakuwa mutego kwenu.
mujue kwa hakika kwamba Yawe, Mungu wenu, hataendelea kuyafukuza mataifa haya mbele yenu, lakini yatakuwa kwenu kikwazo na mutego. Yatakuwa kwenu mujeledi wa kuwapiga na miiba ya kuwachoma kwa macho mpaka pale mutakapoangamia na kutoka katika inchi hii nzuri ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa.
Gideoni akazitumia kwa kutengenezea kizibao ambacho alikiweka kwenye muji wake wa Ofura. Waisraeli wote wakaenda kule kukiabudu. Kizibao hicho kikakuwa mutego kwa Gideoni na jamaa yake.