Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Na kwa upande wenu niliwaamuru musifanye agano na wenyeji wa inchi hii na kwamba mazabahu zao mutazibomoa. Lakini ninyi hamukuitii amri yangu. Kwa nini mambo haya?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 2:2
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme akamwita Abramu, akamwuliza: “Ni kitu gani hiki ulichonitendea? Mbona haukunijulisha kwamba Sarai ni muke wako?


Yawe akasema: “Umefanya nini? Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo.


Musa akamwuliza Haruni: Walikufanya nini watu hawa hata ukawaingiza katika zambi kubwa hivyo?


Na sasa itakufalia nini kwenda Misri kunywa maji ya muto Nili? Au itakufalia nini kwenda Asuria kunywa maji ya muto Furati?


Kwa nini unaniachilia hivi, ukibadilishabadilisha mwenendo wako? Utafezeheshwa na Misri kama ulivyofezeheshwa na Asuria.


Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?


Muangamize taifa lolote ambalo Yawe, Mungu wenu atalitia katika mikono yenu, wala musilionee huruma. Musiabudu miungu yao, maana jambo hili litakuwa mutego kwenu.


katikati ya ndimi za moto kwa kuazibu wale wanaokataa kumujua Mungu na wale wasiokubali Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.


Lakini Waisraeli wakawajibu hao Wahivi: “Tunaweza namna gani kufanya agano nanyi? Labda ninyi munaishi karibu nasi.”


Wakati wa hukumu unakaribia. Na hukumu itaanza na watu wa Mungu. Na kama hukumu inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasiotii Habari Njema ya Mungu?


Kwa hiyo Yawe akawaka hasira juu ya Waisraeli, akasema: “Kwa sababu watu hawa wamevunja agano nililofanya na babu zao, wakakataa kutii sauti yangu,


Kisha nikawakumbusha kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, na kwamba musiiheshimu miungu ya Waamori, ambao inchi yao mumeitwaa, lakini hamukuisikiliza sauti yangu.’ ”


Yawe akawapelekea nabii, naye akawaambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Niliwaondoa katika inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa,


Gideoni akazitumia kwa kutengenezea kizibao ambacho alikiweka kwenye muji wake wa Ofura. Waisraeli wote wakaenda kule kukiabudu. Kizibao hicho kikakuwa mutego kwa Gideoni na jamaa yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ