Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Walimwacha Yawe, Mungu wa wazee wao, ambaye aliwaondoa katika inchi ya Misri, wakaifuata miungu mingine, miungu iliyoabudiwa na watu walioishi kandokando yao. Waliinama mbele ya miungu hiyo, wakamukasirikisha sana Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 2:12
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waliabudu sanamu za miungu yao, nazo zikakuwa mutego wa kuwaangamiza.


Walimukasirikisha kwa mazabahu zao za miungu; wakamutia wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.


Kama kisha mwana wako akiuliza maana ya jambo hili, utamwambia: ‘Kwa nguvu ya mukono wake, Yawe alitutoa katika inchi ya Misri ambako tulikuwa watumwa.


Jambo hili litakuwa kama kitambulisho katika mukono wako au utepe katika paji la uso wako, kwamba Yawe alitutoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.”


Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.


Na mambo haya yatakuwa ukumbusho, kama vile kitambulisho katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; kusudi kiwakumbushe siku zote sheria ya Yawe. Maana, Yawe amewatoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.


Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.


Nawe utawajibu hivi: Babu zenu waliniacha. Wakafuata miungu mingine, wakaitumikia na kuiabudu. Waliniacha, wala hawakuzitii sheria zangu.


Mufuate na kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kushika amri zake na kutii sauti yake. Mumutumikie na kuambatana naye.


Kisha kusikia maneno ya agano hili ambayo mumeapishwa, na mutu akijiamini mwenyewe ndani ya moyo wake na kusema atakuwa salama naye akifuata ugumu wake, hiyo italeta maangamizi.


Wakaenda kutumikia na kuabudu miungu mingine, ambayo hawakuijua mbele, wala Yawe hakukuwa amewapa.


Watu wa usawa walinona, wakapiga mateke. Walinenepa sana, kisha wakamwacha Mungu aliyewaumba, wakazarau Mulima wa wokovu wao.


Utukufu wake ni utukufu wa ngombe dume wa kwanza, pembe zake ni za mbogo dume. Atazitumia kusukuma mataifa; yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia. Efuraimu atakuwa na pembe hizo elfu kumi na Manase kwa maelfu.”


“Mimi leo ninaita mbingu na dunia zishuhudie juu yenu. Mutakapokuwa mukikaa katika inchi hiyo, mukipata watoto na wajukuu na kuwa wazee, kama mukianza kupotoka na kujifanyia sanamu katika umbo la kitu chochote, mukifanya uovu mbele ya Yawe, Mungu wenu, na kumukasirikisha, mara moja mutaangamia kabisa katika inchi ambayo munaenda kurizi huko ngambo ya muto Yordani. Hamutaishi huko muda murefu, lakini mutaangamizwa kabisa.


Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.


muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe aliyewatoa Misri ambako mulikuwa watumwa.


Naye Yawe akawaambia: “Mimi sikuwakomboa kutoka kwa Wamisri, Waamoni, Waamori, na Wafilistini?


Walijichagulia miungu mipya, kukakuwa vita katika inchi. Lakini hakukupatikana mwenye upanga au ngao kati ya watu elfu makumi ine wa Israeli.


Nyuma ya kifo cha Gideoni, Waisraeli wakairudilia miungu ya Bali na kuiabudu. Wakamufanya Bali-Beriti kuwa mungu wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ