Hao ni kama imbwa walafi sana, wala hawawezi kutosheka hata kidogo. Wachungaji nao hawana akili yoyote. Kila mumoja anatafuta njia yake mwenyewe, kila mumoja anatafuta faida yake.
Mumenizaraulisha mbele ya watu wangu kusudi mupate vitanga vya shayiri na chakula kidogo. Munawaua watu wasiostahili kufa na kuwaacha wazima wanaostahili kuuawa, kwa uongo wenu munaowaambia watu wangu, nao wanawaaminia.
Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.
Na kwa sababu ya tamaa yao mbaya ya mali, walimu hawa wa uongo watajipatia faida juu yenu kwa njia ya maneno ya uongo. Lakini tangia zamani hukumu yao imekwisha kutangazwa, nao hawatakawia kuangamizwa.
Mika akamwambia: “Kaa pamoja nami, ukuwe kwangu kama baba na kuhani wangu. Nitakulipa vikoroti kumi vya feza kila mwaka na nguo pamoja na mahitaji yako.”