walimwambia: “Basi useme neno ‘Shiboleti’ ”. Lakini yeye akisema “Siboleti” kwa sababu hakuweza kulitamka sawasawa, walimukamata na kumwua kule kwenye vivuko vya muto Yordani. Watu elfu makumi ine na mbili wa Efuraimu wakapoteza maisha yao wakati ule.
Kwa hiyo watu wa kabila la Dani wakachagua kati yao watu hodari, wakawatuma kutoka kule Estaoli na Zora, wakawaamuru waende kuipeleleza inchi. Basi watu hao wakafika katika inchi ya milima ya Efuraimu katika nyumba ya Mika, wakaenda na kukaa mule.