Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 17:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mika alipomurudishia mama yake hiyo feza, mama yake akatwaa vikoroti vya feza mia mbili akamupatia mufua feza ambaye alifua sanamu ya kuchonga na ya kuyeyushwa. Sanamu hiyo ikawekwa katika nyumba ya Mika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 17:4
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutazihesabu sanamu zenu za miungu zilizopakwa feza na zahabu kuwa uchafu. Mutazitupilia mbali kama takataka, mukisema: Mupotelee mbali!


Vilevile muchoraji wa miti anafanya vipimo vyake kwa kamba, anachapa kitambulisho chake, kisha anatumia vifaa vyake kwa kuchonga. Halafu anatengeneza sanamu na kuipatia umbo la mutu na sura ya kupendeza; kisha anaweka sanamu hiyo ya mungu pahali pake pa pekee.


Sanamu mutu aliyotengeneza inafaa kwa nini? Sanamu ni madini yaliyoyeyushwa, ni kitu cha kueneza udanganyifu! Mutengenezaji wa sanamu anatumainia kile alichotengeneza mwenyewe, sanamu ambayo haiwezi hata kusema!


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayefanya sanamu ya kuchonga au ya kuyeyushwa na kuisimamisha kwa siri, kitu ambacho kimetengenezwa na mikono ya fundi na ambacho ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Mika akamurudishia mama yake hivyo vikoroti vya feza elfu moja na mia moja. Mama yake akasema: “Kusudi laana niliyotoa isikupate, feza hii ninaitoa kwa Yawe kwa kutengeneza sanamu ya kuchonga na ya kuyeyushwa. Sasa ninakurudishia vikoroti vya feza.”


Mutu huyo, Mika alikuwa na pahali pake pa ibada. Alitengeneza kizibao cha kuhani na sanamu, kisha akamufanya mumoja wa watoto wake kuwa kuhani wake.


Wale watu watano waliokwenda kuipeleleza inchi wakaingia ndani, wakabeba ile sanamu ya mungu yenye kuyeyushwa, kile kizibao na sanamu ya ibada. Wakati ule yule kuhani alikuwa akisimama kwenye mulango pamoja na wale watu mia sita wenye silaha.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ