Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 17:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Siku moja akamwambia mama yake: “Vile vikoroti vya feza elfu moja na mia moja ulivyoibiwa, nawe ukamulaani aliyekuiba nami nikiwa ninasikia, mimi niko navyo. Mimi ndiye niliyevibeba.” Mama yake akasema: “Mwana wangu ubarikiwe na Yawe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 17:2
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

akamubariki Abramu akisema: “Abramu abarikiwe na Mungu Mukubwa, Muumba wa mbingu na dunia!


Nikawakaripia na kuwalaani, hata nikawapiga wamoja kati yao na kuwaongoa nywele zao. Nikawalazimisha kuapa kwa jina la Mungu, nikisema: “Wabinti zenu musiwaoeshe kwa vijana wao, wala wabinti zao wasiolewe na vijana wenu au na ninyi wenyewe.


Mwovu anajisifia tamaa zake mbaya, anapata faida kwa njia mbaya, anazarau na kumukataa Yawe.


Usitaje bure jina langu mimi Yawe, Mungu wako, maana mimi Yawe sitaacha kumwazibu yeyote anayetaja bure jina langu.


Anayeiba mali ya baba yake au ya mama yake na kusema si kosa, anatumika pamoja na yule anayeangamia.


Alaaniwe mutu anayefanya kazi ya Yawe kwa uregevu; alaaniwe anayezuia upanga wake usimwange damu!


Halafu Petro akaanza kusema: “Nilaaniwe ikiwa ninasema uongo! Ninaapa kwamba simujui mutu huyu!” Na mara moja jogoo akawika,


Ingekuwa heri nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya wandugu zangu wa damu,


Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe! Bwana wetu, kuja!


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayezarau baba yake au mama yake.’ Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


maana mwenye kumusalimia anashirikiana naye katika matendo yake mabaya.


Kulikuwa mutu mumoja kule katika milima ya Efuraimu, jina lake Mika.


Mika akamurudishia mama yake hivyo vikoroti vya feza elfu moja na mia moja. Mama yake akasema: “Kusudi laana niliyotoa isikupate, feza hii ninaitoa kwa Yawe kwa kutengeneza sanamu ya kuchonga na ya kuyeyushwa. Sasa ninakurudishia vikoroti vya feza.”


Malaika wa Yawe anasema hivi: ‘Ulaani muji wa Merosi, uwalaani vikali wakaaji wake; maana hawakukuja kumusaidia Yawe hawakumusaidia Yawe juu ya wenye nguvu’.


Boazi akasema: “Yawe akubariki, kwa maana kwa yote unayofanya unaonyesha heshima zaidi kuliko uliyoyafanya pale mbele, kwa maana haukuwatafuta vijana wamasikini au tajiri wakuoe.


Siku ile, Waisraeli walisumbuliwa sana maana Saulo alikuwa amewaapiza watu akisema: “Alaaniwe mutu yeyote atakayekula chakula mbele jua kutua, na mbele sijajilipiza waadui zangu kisasi.” Kwa hiyo, siku yote, hakuna mutu aliyeonja chakula chochote.


Mutu mumoja akamwambia: “Baba yako aliwaapiza watu vikali, akisema: ‘Mutu yeyote atakayekula chakula leo alaaniwe.’ ” Nao watu walikuwa wazaifu kwa ajili ya njaa.


Samweli alipomufikia Saulo, Saulo akamwambia Samweli: “Yawe akubariki! Nimetimiza amri ya Yawe.”


Saulo akawajibu: “Ninyi kweli munanionea huruma; Yawe awabariki.


Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ