Basi, Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Muangalie, Yoabu ana shamba la shayiri karibu na langu. Muende mulichome kwa moto.” Kwa hiyo watumishi wa Abusaloma wakalichoma shamba la Yoabu kwa moto.
Basi siku ya ine wakamwambia muke wa Samusoni: “Umubembeleze mume wako kusudi atuambie maana ya kitendawili hicho, kama sivyo tutakuteketeza kwa moto wewe pamoja na nyumba ya baba yako. Ninyi mulitualika hapa kutunyanganya mali zetu?”
Wazazi wake hawakujua kwamba ule ulikuwa mupango wa Yawe ambaye alikuwa anatafuta njia ya kushambulia Wafilistini. Wakati ule, Wafilistini walikuwa wakiwatawala Waisraeli.
akamwambia: “Mimi nilizani kwamba ulimuchukia kabisa. Kwa hiyo nilimwoesha kwa rafiki yako. Hata hivyo, dada yake mudogo ni muzuri kuliko yeye. Tafazali, umwoe huyo kwa pahali pake.”
Basi, Samusoni akaenda, akawakamata mbweha mia tatu naye akawafunga mikia yao pamoja wawili wawili. Kisha akaweka mwenge katika kila mbweha wawili wawili.