17 Alipomaliza kusema, akatupa utaya huo. Pahali pale pakaitwa Ramati-Lehi, maana yake “Mulima wa Utaya”.
Samusoni akaona mufupa mubichi wa taya ya punda, akautumia kuwaua watu elfu moja.
Kisha Samusoni akasema: “Kwa utaya wa punda, nimeua watu elfu moja. Kwa utaya wa punda, nimekusanya malundo ya maiti.”
Kisha Samusoni akashikwa na kiu sana. Basi, akamwomba Yawe, akisema: “Ee Mungu, wewe ndiwe uliyeleta ukombozi huu, kwa kunitumia mimi mutumishi wako. Sasa utaniacha nikufe kwa kiu na kutekwa na Wafilistini hawa wasiotahiriwa?”
Wafilistini wakakuja, wakapiga kambi yao katika inchi ya Yuda na kuushambulia muji wa Lehi.