Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Siku moja, malaika wa Yawe akamutokea yule mwanamuke, akamwambia: “Wewe ni tasa, hauna watoto. Lakini utapata mimba na kumuzaa mutoto mwanaume.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 13:3
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitamubariki, naye atakuzalia mutoto mwanaume. Nitamubariki Sara, naye atakuwa mama wa mataifa mengi na wafalme wa mataifa watatoka kwake.”


Mumoja wao akasema: “Hakika nitakurudilia kwa wakati kama huu katika mwaka na muke wako Sara atakuwa na mutoto mwanaume.” Sara alikuwa kule nyuma kwenye mulango wa hema, akisikiliza.


Kuna jambo lolote lisilowezekana kwa Yawe? Nitakurudilia wakati uliopangwa, kwa wakati kama huu katika mwaka, na Sara atakuwa na mutoto mwanaume.”


Elisha akamwambia: “Mwaka kesho, kwa wakati kama huu, utakuwa na mutoto katika mikono yako.” Mama akamujibu: “Hapana, Bwana wangu! Wewe ni mutu wa Mungu; usinidanganye mimi mutumishi wako!”


Halafu malaika wa Bwana akamutokea Zakaria, akisimama upande wa kuume wa mazabahu ya kuchomea ubani.


Lakini yule malaika akamwambia: “Zakaria, usiogope, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Muke wako Elizabeti atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yoane.


Mwanamuke akakimbia upesi, akamwambia mume wake: “Yule mutu aliyenijia siku ile amenitokea tena.”


Manoa akamwambia huyo malaika wa Yawe: “Tafazali, ukae kidogo tukutayarishie mwana-mbuzi.”


Mwanamuke huyo akaenda kumwambia mume wake: “Mutu wa Mungu ambaye sura yake ilikuwa kama ya malaika wa Mungu alinitokea. Sikumwuliza anatoka wapi wala hakuniambia jina lake.


Kisha Manoa akamwomba Yawe, akisema: “Ninakuomba, ee Yawe, umutume tena yule mutu wako uliyemutuma kusudi atufundishe mambo tunayopaswa kumutendea huyo mutoto atakayezaliwa.”


Malaika wa Yawe aliondoka Gilgali, akaenda Bokimu, akawaambia Waisraeli: “Niliwaondoa katika inchi ya Misri na kuwaleta katika inchi ambayo niliahidi kwa kiapo kwa babu zenu. Nilisema kwamba sitalivunja agano langu nanyi hata kidogo.


Yawe akamugeukia, akamwambia: “Kwenda kwa uwezo unaokuwa nao, uikomboe Israeli kutoka Wamidiani. Ni mimi ninayekutuma.”


Hivyo Hana akapata mimba, akazaa mutoto wa kiume. Hana akamwita mutoto huyo Samweli, maana alisema: “Nimemwomba kwa Yawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ