Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 11:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Basi, Yefuta akawakimbia wandugu zake akaenda kuishi katika inchi ya Tobu. Kule watu wa ovyo wakakusanyika kujiunga naye, wakamufuata katika safari zake za mashambulio.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 11:3
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waamoni walipoona kwamba wamemuchukiza Daudi, walijilipia waaskari wa miguu wa Waaramu elfu makumi mbili kutoka Beti-Rehobu na Zoba, waaskari elfu kumi na mbili kutoka Tobu, na mufalme Maka akiwa na waaskari elfu moja.


Waamoni walitoka na kujipanga tayari kwa vita kwenye mulango wa muji wa Raba, muji wao mukubwa; nao Waaramu kutoka Zoba na Rehobu na watu kutoka Tobu na Maka walijipanga katika mbuga.


Lakini Wayuda wakajaa na wivu, hata wakakusanya watu wamoja wa ovyo ovyo waliowakuta kwenye nafasi za makutano, na kufanya kikundi. Kisha wakafanya fujo katika muji wote. Wakashambulia nyumba ya Yasoni, wakiwatafuta Paulo na Sila kusudi wawapeleke mbele ya watu.


Gileadi alikuwa vilevile na wana wengine toka kwa muke wake. Watoto wa muke huyo walipokuwa wakubwa, wakamufukuza Yefuta kutoka kwao, wakamwambia: “Wewe hauna haki ya kupata urizi kutoka kwa baba yetu, maana wewe ni mutoto wa mwanamuke mwingine.”


Wakamupa vikoroti makumi saba vya feza vilivyokuwa kwenye nyumba ya Bali-Beriti ambavyo alivitumia kwa kulipa watu wakorofi na watu ovyoovyo kusudi wamufuate.


Watu wote waliogandamizwa au waliokuwa na madeni au wale wenye huzuni walijiunga na Daudi. Jumla yao ilikuwa watu yapata mia ine, naye akakuwa kiongozi wao.


Kwa hiyo, mara moja Daudi na watu wake mia sita wakaenda kwa Akisi mwana wa Maoki, mufalme wa Gati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ