Namani, jemadari wa waaskari wa mufalme wa Aramu, alikuwa mutu mukubwa aliyeheshimiwa sana na bwana wake, maana kwa njia yake Yawe aliiletea inchi ya Waaramu ushindi. Alikuwa askari hodari, lakini alikuwa na ugonjwa wa ukoma.
Waisraeli na viongozi wao wakaulizana: “Ni nani atakayeanza kupigana na Waamoni? Atakayefanya hivyo ndiye atakayekuwa kiongozi wa wakaaji wote wa Gileadi.”
Gileadi alikuwa vilevile na wana wengine toka kwa muke wake. Watoto wa muke huyo walipokuwa wakubwa, wakamufukuza Yefuta kutoka kwao, wakamwambia: “Wewe hauna haki ya kupata urizi kutoka kwa baba yetu, maana wewe ni mutoto wa mwanamuke mwingine.”
Halafu Yawe alimutuma Yerubali, na kisha akamutuma Bedani, kisha Yefuta, na kwa mwisho akanituma mimi Samweli. Kila mumoja wetu aliwaokoa kutoka waadui zenu waliowazunguka, nanyi mukaishi kwa amani.