Yairi alikuwa na watoto wa kiume makumi tatu ambao walipanda juu ya punda makumi tatu na walikuwa na miji makumi tatu katika inchi ya Gileadi, ambayo mpaka leo inaitwa Miji ya Yairi.
Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.