Wakati ule, Yoshua akakwenda, akawaangamiza Waanaki waliokuwa wanaishi katika milima kule Hebroni, Debiri, Anabu, inchi yote ya milima ya Yuda na Israeli. Yoshua akawaangamiza watu hao pamoja na miji yao.
Inchi hizo zilikuwa pamoja na maeneo ya milima, inchi ya bonde, eneo la Araba, miteremuko ya milima, maeneo ya jangwa, na eneo la Negebu; inchi zilizokuwa za Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Waliwashambulia vilevile Wakanana walioishi katika muji wa Hebroni ambao zamani uliitwa Kiriati-Arba, wakashinda makabila ya Sesai, Ahimani na Talmayi.